Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa maji Mitaa yote ya Kata za Mbezi Juu, Wazo na Mabwepande katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, muuliza swali alisisitiza ukosefu wa maji katika maeneo ambayo ameyataja ya Mabwepande, Wazo pamoja na Mbezi Juu. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itaongeza speed ya kumaliza hiyo kazi ili wananchi Waheshimiwa Wabunge, pale waweze kupata hayo maji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mradi wa Maji kutoka Masoko katika Wilaya ya Rungwe unafanana kabisa kama ambavyo wanahangaika watu wa Wazo.

Je, ni lini watahakikisha watu wa vya Kasyeto, Mpumbuli pamoja na Segela wanapata maji kwa sababu ilipoanzishwa maji katika Mto Masoko tulitegemea sana watu wa maeneo haya wapate maji safi na salama na kwa wakati sahihi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge Viti Maluum, yaliyoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Sophia Mwakagenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lini Serikali itaongeza kasi? Tayari tumejipanga na na kuanzia sasa tunaongeza kasi na kuhakikisha maeno haya yote tunakwenda kuyafikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Mradi wa Masoko Rungwe, Mheshimiwa Mbunge ni shahidi mimi na yeye tulishawahi kuongea tukiwa Mbeya na hili tutalifanya pamoja mimi na yeye baada ya Bunge hili na kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo, tutahakikisha hili suala la Mradi wa Masoko sasa linafikia mwisho wake.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa maji Mitaa yote ya Kata za Mbezi Juu, Wazo na Mabwepande katika Jimbo la Kawe?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya wakazi wa Jiji la Arusha kuletewa bili za maji tofauti na matumizi yao na hivi juzi Mamlaka ya Maji ya Jiji la Arusha imetangaza kuongeza gharama za maji kuanzia kesho. Je nini kauli ya Serikali?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge Viti Maalum kutoka Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipende kumpongeza amekuwa akifuatilia sana suala la hizi bili za maji kwa Jiji la Arusha na maeneo yote. Hata hivyo, kwenye suala la ongezeko la bei ambaho imetangazwa hapo kesho ni utaratibu tu ambao upo kikanuni na tayari EWURA waliweza kufuata taratibu zote na kushirikisha wananchi kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara ambayo iliweza kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na manung’uniko haya sisi kama Wizara tumelipokea na kuona namna gani tutalifanya. Lengo ni kuona huduma za maji zinabaki kuwa endelevu na zinaboreshwa kwa kutumia hizi fedha zinazochangiwa na wananchi, lakini vile vile kuhakikisha wananchi wanatumia katika gharama tunaziweza.