Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Igalula?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze Serikali kwa majibu mazuri. Ni kweli Wilaya ya Uyuwi tumepata chuo cha VETA, lakini kutokana na jiografia ya Wilaya ya Uyuwi na kuwepo kwa majimbo mawili, wananchi wa Jimbo la Igalula kwenda kuifata VETA ni zaidi ya kilometa 200.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kunipatia upendeleo maalum wa kunipatia angalau hata shule ya ufundi ili niweze kuwa na shule ya ufundi na wanachi wa Jimbo la Igalula wakanufaika na matunda ya Mama Samia Suluhu Hassan?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti,kama nilivyoeleza kwenye majibu ya swali la msingi kwamba ni azma ya Serikali kujenga vyuo hivi katika wilaya zote ikiwemo Wilaya ya Uyuwi, hivyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali wakati inajenga miundombinu hii vile vile tunatoa huduma za mabweni pamoja na zile za kutwa. Lakini vile vile tunafahamu, inawezekana huduma hizi za mabweni kwa wale wanafunzi wanaotoka mbali zinaweza zikawa sio toshelezi. Serikali vile vile inatambua kwamba kuna Wilaya ambazo ni kubwa na jiografia yake ni kubwa na zina majimbo zaidi ya moja. Nitoe tu mfano wa hiyo Wilaya ya Uyuwi lakini tuna Wilaya ya Bagamoyo, tuna Wilaya ya Lindi kuna Wilaya ya Bariadi kwa hiyo kuna Wilaya nyingi ambazo zinachangamoto aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, tunauchukua ushauri wake. Serikali ina mipango mingi endelevu na Serikali hii ya Mama Samia tunakwenda kufanya mambo makubwa kwa lengo la kusogeza huduma za elimu pamoja na elimu ya ufundi karibu. Kwa hiyo andaa tu eneo kwa ajili ya ujenzi wa hiyo shule uliyozungumza na Serikali ya Mama Samia ni sikivu. Tuna amini baada ya kukamilisha ujenzi wa vyuo hivi tunakwenda sasa katika ujenzi wa shule hizi za ufundi katika maeneo ambayo yamekosa vyuo vya VETA, nakushukuru sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Igalula?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa mpango Mkakati wa kujenga Vyuo vya VETA kila wilaya. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kujenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Simanjiro?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia, Mbunge kutoka Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Simanjiro wenzetu wa Taasisi ya Upendo walijenga chuo kilikuwa hakijakamilika miundombinu yake lakini baada ya kujenga waliikabidhi Serikali. Chuo ambacho kipo katika Wilaya ya Simanjiro kipo katika Kijiji Engalakash katika Kata ya Emboret, lakini kilikuwa kimejengwa kweli na wenzetu wa Upendo na wamekwisha kabidhi Serikali na kilikuwa na miundombinu ifuatayo: Karakana mbili; Madarasa; Bwalo; Mabweni mawili; na Kisima cha maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha Serikali imepeleka pale milioni 190 kwa ajili ya kuongeza miundombinu ambayo tunakwenda kujenga Bweni moja, tunajenga nyumba za watumishi, lakini kulikuwa na changamoto za umeme. Kwa hiyo, tunasambaza umeme ndani ya majengo pamoja na nje ya majengo na tutaendelea kufanya hivi. Kwa hiyo, sasa hiki ndiyo kitakuwa Chuo cha Wilaya ya Simanjiro kinachomilikiwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwondoe hofu tutaendelea kuongeza majengo kama tunavyofanya katika maeneo mengine kama vile Urambo, Nanyumbu na maeneo mengine ambayo tulikuwa na vyuo vya zamani vilikuwa na miundombinu ambayo sio toshelezi, tutakwenda kujenga miundombinu ili kutosheleza kutoa huduma ile ya VETA katika maeneo yote ya wilaya zote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.