Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la ukosefu wa dawa kwa wazee wanaopata huduma ya matibabu bure katika hospitali nchini?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa sasa Serikali imekiri kwamba kuna tatizo kubwa la upungufu wa madawa kwenye zahanati;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa wazee bima maalum ya afya ambayo inaweza ikawasaidia kupata dawa katika maduka ya watu binafsi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa sasa kuna mmomonyoko wa maadili miongoni mwetu kijamii wazee wakiwa wanaenda hospitali wengi hawawapishi katika zile foleni wanawaacha wazee wanapata shida.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kila hospitali inakuwa na madirisha maalum ya wazee kupata huduma haraka?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake hili muhimu sana kwa ajili ya afya za wazee wetu. Kwanza nianze kwa kumwambia Mheshimiwa Mbunge, moja tuliposema tunakuja na Bima ya Afya kwa Wote, ndilo lilikuwa suluhisho la hili jambo, na unajua kwamba kwenye Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote tulikuwa na kipengele cha kuwalipia watu wasio na uwezo, kwamba wanakuwa na bima ya afya, maana yake na kuwa wazee wako sehemu ya hili. Lakini suala la kusema kwamba wapate bima maalum ili wakikosa ndani ya hospitali zetu dawa waweze kupata kwenye maduka binafsi; mimi nafikiri cha msingi hapa ni hospitali zetu, kwa maana ya vituo vya afya, hospitali za wilaya na zahanati zetu ziwe na dawa zote ambazo zinaweza kuwasaidia wazee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mikakati imefanyika; nafikiri Mheshimiwa Mbunge unajua jinsi ambavyo sasa hivi dawa zikifika kuna kamati za vijiji za kupokea dawa, Waheshimiwa Wabunge wanapewa ripoti na kila mtu anashiriki kwenye mchakato huu. Nina hakika hakutakuwepo na upungufu mkubwa na wazee watapata dawa zao.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la ukosefu wa dawa kwa wazee wanaopata huduma ya matibabu bure katika hospitali nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali la nyongeza fupi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Vunjo kuna vituo vya afya vinne tu licha ya kwamba tuna kata 16. Na hivi vituo vya afya vikiwemo Unyika Msae, Marangu Head Quarter ambacho ni kipya, Kilua Vunjo na Kahe havina uwezo wa kutoa huduma ya upasuaji, hususan kwa wanawake ambao ni wajawazito na hivyo wanalazimika kupewa rufaa kwenda kwenye hospitali za Mawenzi ambapo ni mabli au KCMC ambapo pia kuna usumbufu mkubwa;

Je, ni lini Serikali itatoa vifaa na madaktari ili vituo hivi viweze kutoa huduma hiyo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Serikali ya Doctor Samia Suluhu Hassan ilipopeleka vituo vya afya kule kwa kweli lengo lake ni kufika mahali vile vile viweze kufanya upasuaji waweze kuwasaidia akina mama kule kule badala ya kuwapeleka mbali kama hospitali ya Mkoa anavyosema Mheshimiwa. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge kama suala ni ukosefu tutakuja kuangalia vituo vyako specifically kama theater ipo na vitu vingine vipo. Kama ni ukosefu wa vifaa tutashirikiana na wenzetu TAMISEMI tuone namna vitakavyoweza kupatikana ili huduma hiyo iweze kutolewa.