Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza kwa kuwa kuna uhaba mkubwa sana wa ardhi maeneo ya Kata ya Luponde ambako ndiko shamba kubwa hilo lipo na mashamba makubwa ya chai yako kule, na vijana ni wengi sana ambao wanauhitaji wa ardhi;

Je, kwa nini Serikali isifikirie ndani ya eneo hili ikagawa sehemu kuwapa vijana katika mpango wa BBR au BBT?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kituo cha utafiti cha Igeri ambacho ndicho kimekuwa na shamba hili kwa muda mrefu sana kimekuwa dormant kwa miaka mingi sana hakujakuwa na uwekezaji, na vile vile kituo kidogo cha Ichenga ambacho ni cha utafiti eneo hilo hilo na chenyewe cha matunda kimekuwa dormant na hakina fedha na hakifanyi shughuli yoyote wakati tuna zao la parachichi ambalo linahitaji sana utafiti;

Je, Serikali ina mpango gani kutoa fedha za kutosha kwenye vituo hivi vya utafiti?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza kuhusu vijana na ushiriki wa vijana kwenye kilimo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba ni dhamira ya Serikali kuhakikisha vijana wengi zaidi wanashiriki kwenye kilim,o na ndio maana tumekuja na programu ya BBT. Na kwa kuwa kuna changamoto ya ardhi kama alivyosema, mimi nitaandaa safari kwenda jimboni kwake Mheshimiwa Mbunge tukakae na uongozi wa wilaya kwa pamoja tutafute namna bora ya kuweza kuwawezesha vijana hao washiriki kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuhusiana na kituo hiki cha utafiti. Kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, mwaka wa fedha unaokuja wa 2023/2024 tumetenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunalima eneo lote kwa ajili ya kutayarisha mbegu zile ambazo ni pre-basic seeds na basic seeds ili baadaye tusaidie kwa ajili ya kuzisambaza, hasa kwenye zao la ngano na zao la pareto. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba hatujakitelekeza, tumeshakitengea fedha, kitaanza kuwa operational kuanzia mwaka wa fedha ujao.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa changamoto kubwa ya wakulima wetu nchini ni upatikanaji wa mbegu bora; je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mbegu bora zinapatikana kwa wakati ukiwemo Mkoa wangu wa Iringa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mkakati wa Serikali kwa kutumia Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA) na wazalishaji binafsi kuhakikisha tunazo mbegu za kutosha kuweza kuwahudumia wakulima wa nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya mbegu za kilimo katika mpango wetu ule wa Agenda kumi thelathini ifikapo mwaka 2030 ni kuwa na uzalishaji wa tani takriban laki sita na Hamsini elfu. Hivi sasa tupo katika uzalishaji wa tani 61,000 kama asilimia kumi ya mahitaji yetu katika mwaka 2030.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, hivi sasa kwenye mashamba yetu yote ya ASA tumeweka mifumo maalum ya umwagiliaji ambayo itatuhakikishia uzalishaji wa mbegu zaidi ya mara mbili ndani ya mwaka mmoja, na hivyo wakulima wetu watapata mbegu kwa wakati kwa sababu hivi sasa tumeboresha mashamba yetu 16 na mbegu zitaanza kuzalishwa zaidi ya mara moja ndani ya msimu.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wilaya ya Chemba imetenga maeneo kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu na tafiti, na tunafahamu Taifa hili lina changamoto ya upungufu wa mbegu;

Je, nini mkakati wa Serikali wa kuyatumia maeneo haya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kwa utayari wao wa kutenga ardhi kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu na utafiti. Hivi sasa tuko nao katika mazungumzo ya mwisho kwa ajili ya kuanza kuanzisha shamba kubwa la uzalishaji wa Mbegu za mtama mfupi ambao una soko kubwa kwa kampuni ya bia Tanzania pamoja WFP na wakulima wakubwa wanapatikana ndani ya Mkoa wa Dodoma na Singida. Kwa hiyo shamba hili ndani ya Chemba litakuwa kama mwokozi kwa wakulima wa kanda ya kati.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia vijana wa Wilaya ya Nyang’hwale kupitia mpango wake wa kuwanyanyua vijana kupitia kilimo? Wilaya ya Nyang’hwale hatuna mazao ya kudumu ya kibiashara; je, Serikali ina mpango gani wa kuchukua udongo na kufanya utafiti ili na sisi tuweze kuwa na miche ama mazao ya kibiashara?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mkakati wa Serikali wa kuhakikisha ya kwamba tunawahusisha vijana wengi kwenye kilimo na ndio maana tumekuja na programu hii ya BBT. Hatua ya awali ambayo tunaifanya kwanza kabisa tunashirikiana na mamlaka za mikoa husika kwa ajili ya utengwaji wa maeneo; na eneo la pili hivi sasa tumeanza kuichora ramani ya Tanzania kwa afya ya udongo ili tujue sehemu gani wanaweza kulima zao gani na sisi tuwasaidie jambo gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, habari njema ni kwamba katika mwaka ujao wa fedha tumekwenda kununua mitambo ya kisasa ya upimaji wa afya ya udongo. Badala ile ya mahabara tu tutakuwa pia na mobile laboratory ambazo zitakuwa zinatembea kupima afya za udongo. Tukija kukupimia kwako mkulima tutapima hapo hapo na nitakupa cheti hapo hapo kitakwambia kwamba katika udongo huu unaweza kulima mazao ya aina gani na utumie mbolea aina gani, na hiyo ndio itakuwa mkombozi kwa wakulima wan chi yetu ya Tanzania.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wilaya ya Kishapu na Mkoa wa Shinyanga unajihusisha sana na kilimo cha zao la kimkakati la pamba, lakini zao hili katika msimu huu limeshuka sana bei, kutoka shilingi 2,200 hadi shilingi 1060. Wakati huo gharama kubwa za uendeshaji ama uzalishaji wa zao hili umekuwa ukiongezeka ikiwemo pembejeo na gharama zingine;

Je, ni nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba inafanya kila jitihada kuona kwamba bei hii inapanda ili kumtia moyo na kumhamasisha mkulima ilimradi aweze kuondokana na gharama ya uendeshaji wa zao hili na hivyo kupata manufaa kutokana na zao hili la pamba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya bei ya mazao mengi hapa nchini inatokana na kwamba wakulima wetu wanatumia nguvu kubwa ya wanachokiingiza shambani na wanachokipata havilingani. Sisi kama Serikali tumekuja na mkakati ufuatao. Tunaamini kabisa mkulima wa Tanzania akilima kwa tija suala la bei halitakuwa changamoto kubwa sana. Kwa hiyo mkakati wetu wa kwanza kabisa wa kuanzia ni kuhakikisha kwamba wakulima wetu wanalima kwa tija na hivyo tumefanya yafuatayo;

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza tunasaidia kuendelea kufanya utafiti kwa ajili ya kuwapatia mbegu bora, cha pili ni kuwasaidia pia katika teknolojia ambayo itamsaidia mkulima aweze kulima kwa tija, na cha tatu ni usambazaji wa pembejeo kwa wakati ili mkulima aweze kufikia malengo yake. Hii itatusaidia sana kwenye kuhakikisha kwamba wakulima wetu wanalima kwa tija na hatimaye hata akienda sokoni bei ikiwa imeporomoka lakini atakuwa na uwezo mkubwa wa kuweza kufidia changamoto ambayo anaipata katika uwekezaji alioufanya shambani.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Supplementary Question 6

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali;

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga benki ya kuhifadhi mbegu asilia zisije kupotea kabisa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mamlaka ya afya mimea na viuatilifu pale Arusha tayari tunayo benki ya uhifadhi wa mbegu za asili, na tunaendelea kufanya utafiti. Lengo letu ni kuzitunza na kuhakikisha kwamba zinaendelea kutumika na kuwaletea tija wakulima wetu wa nchi ya Tanzania.