Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Mradi wa TACTIC utaanza Singida Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Napenda kufahamu: Je, mradi huu utazingatia ujenzi wa soko la vitunguu na Soko Kuu la Ipembe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sima ambalo limeulizwa kwa niaba yake, mradi huu unazingatia miradi ile ambayo ilipendekezwa na Halmashauri za Manispaa, Halmashauri za Majiji na Town Councils wenyewe. Kwa hiyo, huwa mapenekezo yanaletwa kwa wenzetu wa TARURA kupitia waratibu wa mradi huu wa TACTIC. Yanapoletwa, basi wanachambua na 30 percent ya miradi ile iliyoletwa, ndiyo ambayo inapitishwa na kutengewa fedha. Kwa hiyo, kama wao wenyewe Manispaa walileta soko hili la vitunguu na soko kuu, basi naamini itakuwemo katika mradi huu wanapopatikana hao Consultants kufanya usanifu.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Mradi wa TACTIC utaanza Singida Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri; je, Manispaa ya Moshi katika Mradi huu wa TACTIC itaanza lini? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotoa maelezo kwenye majibu yangu ya msingi, hivi sasa wapo katika kuwapata consultants wa ku-design miradi hii na pale watakapopatikana, basi designs zitafanyika na ndipo mradi huu utaanza mwisho wa mwaka wa fedha 2023/24.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Mradi wa TACTIC utaanza Singida Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mradi huu pamoja na mambo mengine utahusisha ujenzi wa miradi ambayo itakuwa chanzo cha mapato katika hiyo miji 45; na kwa kuwa huu ni mkopo: Je, Serikali haioni umuhimu wa kukaa na Benki ya Dunia ili awamu ya pili na awamu ya tatu zote zikaenda pamoja ili utekelezaji wa mradi huu uanze mapema? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tunalipokea. Tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha ambao ndio wanzungumza na World Bank kuona kama hili linaweza likafanyika, lakini kwa sababu ya ukubwa wa miradi hii ni lazima iende kwa awamu ili kuhakikisha monitoring ya miradi hii inakuwa ni nzuri ili fedha zinazoletwa, kama alivyosema yeye mwenyewe, Mheshimiwa Chumi, kwamba ni mkopo, hivyo basi Watanzania watalipa, zisitumike vibaya. Kwa hiyo, ni vyema tuka-monitor miradi hii kwa awamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Chumi kwamba miradi hii itafika katika maeneo yote ya majiji haya 45 kwa wakati ambao umepangwa.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Mradi wa TACTIC utaanza Singida Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni lini sasa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni nayo itaingizwa kwenye Mradi wa TACTIC? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, tukimaliza tathmini ya hizi tier tatu za miji hii 45, ndipo tutaangalia kama Serikali kuona uwezekano wa kuongeza Miji, Halmashauri za Manispaa na Halmashauri nyingine DC ambazo zipo nchini, ikiwemo ya Manyoni. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute subira, na pale ambapo tutakamilisha mchakato huu, kama nilivyokuwa nimemjibu Mheshimiwa Chumi, basi tutaangalia na maeneo mengine ya nchi yetu.