Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuubadilisha Mkoa wa Dar es Salaam kwa kujenga barabara za mitaa, mifereji na miundombinu mingine?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH M. MASABURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ambayo sijaridhika kidogo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na bajeti kuwa ndogo ambayo haikidhi mahitaji halisi ya barabara za Mkoa wa Dar es Salaam, ukizingatia Dar es Salaam ina wakazi wengi ambao unaweza kulinganisha na Mikoa minne, mitano ama sita katika nchi hii.

Je, Serikali haioni haja ya kuunda mamlaka itakayoshughulika na barabara za Mkoa wa Dar es Salaam? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa, Mkoa wa Dar es Salaam hatuna ruzuku ya pembejeo, mbolea, shida yetu ni barabara, mifereji, madaraja, labda na panya road.

Je, Serikali haioni huruma kwa adha wanayoipata wananchi kwa kuhangaika na ukizingatia sasa hivi barabara nyingi zimejengwa kutokana na ujenzi wa reli na barabara zile za BRT? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Massaburi:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bajeti ndogo kwa Barabara, nimuarifu Mheshimiwa Masaburi kwamba ni jitihada za Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha barabara za Jiji la Dar es Salaam zinapitika wakati wote na kutengenezwa kwa kiwango cha lami, kwanza kwa kuweka shilingi bilioni 800 na zaidi ya hapo katika Mradi wa DMDP I.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa siku hizi mbili hapa Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Angellah Kairuki, amewakaribisha Wabunge wote wa Dar es Salaam kwenda kushuhudia utiaji saini wa mikataba ya consultants katika mradi wa DMDP II ambapo nao ni commitment kubwa ya Serikali katika Jiji la Dar-es-Salaam, kuhakikisha barabara zote zinapitika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninakuomba Mheshimiwa Massaburi uwe na subira na wananchi wa Dar es Salaam Serikali inaweka fedha zaidi tena ya bilioni 800 katika kutengeneza miundombinu mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili la kwa nini Serikali isiongeze miundombinu kama reli na kadhalika. Hili tunalipokea kama Serikali na tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi kuona ni nanma gani tutaboresha zaidi miundombinu, lakini tayari kama nilivyosema hapo awali katika mradi huu wa DMDP II, Dar es Salaam inakwenda kupendezeshwa chini ya Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha barabara zinapitika, mito inajengwa vizuri na mifereji ya kupitisha maji ili wananchi wa Dar es Salaam waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi bila kupata bughudha yoyote ya kiusafiri.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuubadilisha Mkoa wa Dar es Salaam kwa kujenga barabara za mitaa, mifereji na miundombinu mingine?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Dar es Salaam ni Mkoa mkubwa na ni Jiji la kibiashara, kwa kuzingatia vigezo vyote, kwa maana ya idadi ya watu, kiuchumi na idadi ya magari ni kubwa sana. Je, nini mtazamo wa Serikali wa kuanzisha Mamlaka ya Usimamizi na Kuendeleza Jiji la Dar es Salaam kwa maana ya Dar es Salaam Metropolitan Authority?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ndugulile la kwa nini Serikali isianzishe Mamlaka ya Usimamizi wa Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tunalipokea kama ushauri na tayari Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa maelekezo yake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Angellah Kairuki, kuna timu ambayo inaliangalia hili na kuona ni namna gani linaweza kufanya kazi, pale timu hii itakapowasilisha ripoti hii kwa Mheshimiwa Waziri, basi tutaona hatua zinazifuata za kuchukuliwa.

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuubadilisha Mkoa wa Dar es Salaam kwa kujenga barabara za mitaa, mifereji na miundombinu mingine?

Supplementary Question 3

MHE. TUMAINI B. MAGESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara, mitaro na madaraja katika Mji Mdogo wa Katoro ni mibovu, katika Kata tatu za Ludete, Nyamigota na Katoro yenyewe. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba miundombinu hiyo inatengenezwa ili wananchi waweze kuhudumiwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba, taasisi yetu ya TARURA ambayo inasimamia barabara za Mijini na Vijijini inakuwa na fedha ya kutosha kwa ajili ya kutengeneza barabara hizi, zikiwemo za Mji Mdogo wa Katoro, ndiyo maana Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeiongezea fedha TARURA mara tatu ya bajeti iliyokuwepo 2021. Hivyo, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuona katika barabara hizi za Mji Mdogo wa Katoro kama zimetengewa fedha kwenye mwaka huu wa fedha tunaoenda kuuanza Julai na kama hazijatengewa fedha basi tutahakikisha zinatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuubadilisha Mkoa wa Dar es Salaam kwa kujenga barabara za mitaa, mifereji na miundombinu mingine?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Ukerewe limekuwa likipata wakati mgumu sana wa kupata Wakandarasi na Wakandarasi kushindwa kuja Ukerewe kwa sababu ya gharama kubwa ya kusafirisha vifaa vyao. Nini mkakati wa Serikali wa kuichukulia Ukerewe kama eneo maalum la kibajeti kwa ajili ya barabara? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, tayari kuna timu ambayo inafanya tathmini kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuangalia jiografia ya nchi yetu, kuona bajeti inayopelekwa kwa ajili ya barabara na kama kuna uwiano ambao ni sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, timu ile tayari ilikuwa imemaliza kazi yake na sasa imepelekwa kwa independent consultants kuweza kuiangalia vilevile taarifa ile na kisha mapendekezo yale yakirudi basi formula ya kutoa fedha iweze kubadilika kadri ya mapendekezo ambavyo yatakuja kwa ajili ya utengenezaji wa barabara. Hivyo, basi nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge kwamba, naamini katika maeneo yenye jiografia ngumu ya ufikaji kama ya Ukerewe na yenyewe timu hii itakuwa imeangalia hayo matatizo ambayo yapo. (Makofi)