Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanzisha Vituo Maalum vya Masuala ya Uwekezaji na Masoko kwa Wanawake katika kila Kata?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nilikuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza: Je, Serikali haioni haja sasa ya kuwasaidia wajasiriamali wadogo kutafuta masoko nje ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Nini mkakati wa Serikali kuwaandaa wajasiriamali hawa wadogo kuwa wawekezaji ndani ya nchi yao? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuwatafutia masoko nje ya nchi, ndiyo maana utaona kuna majukwaa mbalimbali ya akina mama pamoja na makongamano yanayowakutanisha wafanyabiashara wanawake na wakati mwingine husafirishwa kwenda katika nchi mbalimbali kuhudhuria makongamano kama hayo kama njia ya kuwajengea uwezo na kutafuta masoko kwa ajili ya bidhaa wanazozalisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili la kuwawezesha wawe wafanyabiashara wakubwa, nimesema katika jibu la msingi kwamba Serikali imetoa fursa mbalimbali za kuwakopesha wafanyabiashara wakiwemo akina mama ili waweze hatimaye kuimarisha mitaji yao kuikuza na hatimaye wawe wafanyabiashara wakubwa. Ni matarajio yetu fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali hususan hii Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan itawezesha akina mama kuendelea kuongezeka katika idadi ya wafanyabiashara wakubwa katika nchi yetu, nakushukuru sana.