Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kujenga kivuko cha juu barabara ya njia nane eneo la Magari Saba Mbezi ili kulinda uhai wa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nitumie nafasi hii kuishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita kutekeleza miradi yetu kwa haraka sana, lakini pamoja na hilo naomba niulize maswali au maombi mawili kwa Serikali.

Mheshimiwa Spika, moja, hapo ambapo tumewekewa kivuko cha pundamilia na taa sasa hivi tunavuka salama, lakini inatubidi tutembee mita sabini pembezoni mwa barabara ili tuingie kwa Musuguri ambapo jioni tunagongwa sana na magari. Ni ombi kwa Serikali, haioni sababu au haja ya kutengeneza Barabara ya wapita kwa miguu katikati ya road reserve ili tuweze kuingia kwa Musuguri kwa usalama?

Mheshimiwa Spika, pili, kwa chini hapa kwenye makutano ya Magari Saba na Mbezi kuna kivuko kingine ambacho Serikali imeanza kukijenga kwa kuweka taa, lakini imekiacha kwa muda mrefu. Je, ni lini Serikali itakamilisha taa zile ili nah apo wananchi wavuke kwa usalama?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mawili ya nyongeza na pongezi.

Mheshimiwa Spika, hili suala ni la utekelezaji. Naomba nichukue nafasi hii kumuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na TANROADS Makao Makuu waende wakaone uwezekano wa haya mawazo ya Mheshimiwa Mbunge kuona namna watakavyofanya ili wananchi waweze kutumia haya maeneo ya road reserve ili waweze kupita kwa usalama katika eneo hili. Hili ni suala la utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, na suala la pili pia ni utekelezaji kwa sababu, mkandarasi yuko site, waweze kumsimamia na kuhakikisha kwamba, anakamilisha kazi ambayo anaendelea nayo ya kukamilisha mataa, ili kuweza kuleta usalama hapa katika hii barabara ya njia nane. Ahsante.