Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, Serikali inatambua utaratibu wa Mgodi wa GGML wa ku-blacklist vijana nchini na ni vijana wangapi wapo blacklisted?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pia naomba kumshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu, nina maswali mawili ya nyongeza.

La kwanza, kwa kuwa upo ushahidi kwamba hiki kinachoitwa taarifa kimekuwa kikitumika na kinaendelea kutumika kuwanyima haki Watanzania ambao hata kama walikutwa na tatizo dogo tu, kufanya kazi katika migodi yote mikubwa Tanzania. Serikali ipo tayari kulitolea maelekezo?

Mheshimiwa Spika, la pili, kwa kuwa taarifa hizi ambazo zimeitwa taarifa, naita blacklisting, zinapomkuta Mtanzania zinadumu milele kinyume na Sheria ya Makosa ya Jinai. Mtu anapotuhumiwa anaadhibiwa na baadaye anakuwa Mtanzania huru.

Je, Serikali ipo tayari kutoa maelekezo ili makosa haya yasiwaadhibu Watanzania milele, wasiajiriwe popote pale katika migodi? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge Kanyasu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza la kuhusiana na kwamba anao ushahidi wa matendo haya kutokea. Namuomba Mheshimiwa Mbunge Constantine Kanyasu, anipatie ushahidi huo kama tulivyoahidi kwenye majibu yangu ya msingi ili tuweze kuhakikisha haki za Watanzania hawa zinatendeka kwa sababu, Serikali ni wajibu wetu kulinda pande zote na sisi ndiyo wasimamizi na custodian wa sheria lakini pia usimamizi wa Haki za Binadamu.

Mheshimiwa Spika, ni kinyume kama kweli itakapoonekana ushahidi upo, unaothibitisha kwamba hao watu wametendewa kinyume na kutumia arbitrariness procedures ambazo na pengine wakati mwingine discretional powers ambazo waajiri wao wanakuwa wanazitumia kuwagandamiza Watanzania. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, nipate orodha hiyo, na mimi na yeye tutafanya kazi hiyo na ninamuahidi tutafika kwenye mgodi husika ambao ameulalamikia.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu kosa kuwa milele. Ni principle yetu kwamba mtu atatuhumiwa lakini pia utaratibu utafanyika wa kuthibitisha kosa hilo. Kama ni la jinai, itakuwa beyond reasonable doubt na kama ni kosa la dawa, itakuwa ni on balance of probability. Sasa yale ambayo yamethibitika beyond reasonable doubt na hatua zikachukuliwa, maana yake ukishatoa adhabu, haihesabu tena kosa hilo kuja kutumika.

Mheshimiwa Spika, ni kosa kisheria kufanya hivyo, hilo nalo pia ninalichukua na nampongeza Mheshimiwa Mbunge kama amebaini hayo ili tuwatendee haki Watanzania ambao lazima washiriki katika ujenzi wa Taifa lao na kufanya kazi kwa ajili ya nchi hii, ahsante.