Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa juhudi kubwa za Serikali kwenda kutujengea Mahakama ya Wilaya kule Nachingwea. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kuna upungufu mkubwa wa Watumishi katika Idara ya Mahakama Wilaya ya Nachingwea; je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza watumishi kwa ajili ya kuboresha ufanisi wa kazi? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa Hakimu mmoja anahangaika kuhudumia Mahakama ya Mwanzo zaidi ya tano, lakini fedha za kuhudumia shughuli za Mahakama hazitoshi; je, Serikali ina mkakati gani kuongeza fedha kila mwezi kwa ajili ya shughuli za Mahakama? Ahsante. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ungele kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ninakiri ni kweli tuna upungufu wa watumishi katika Muhimili wetu wa Mahakama kama ambavyo upungufu huu upo katika Serikali kwa maeneo mbalimbali. Ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa akituongezea watumishi katika Muhimili wetu wa Mahakama, na ninyi ni mashahidi ndugu zangu ni majuzi tu ametuteulia Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu na kadhalika, tunaendelea kuomba kupeleka vibali kwa ajili ya nyongeza ya watumishi.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Nachingwea ni kweli wana upungufu wa watumishi. Primary Court (PC) ambazo zina Mahakimu ni tatu, Primary Court ambazo zinahudumiwa na hao Mahakimu watatu ni watano. Mheshimiwa Mbunge nikuhaidi kwamba tutaendelea kuwasiliana ndani ya Serikali kuongeza Mahakimu katika Mahakama hizo ili huduma iweze kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anazunguzia suala la nyongeza ya fedha, kwamba hawa watumishi wanapokuwa wanatoka maeneo hayo kuhudumia Mahakama zile ambazo inabidi waende, kwa kuwa Mahakimu hawajafika wanahitaji fedha kwa ajili ya kuhudimia.

Mheshimiwa Spika, nishukuru Bunge lako Tukufu, nimshukuru Mheshimiwa Rais kwamba mhimili wa Mahakama umekuwa ukiongezewa fedha. Mwaka huu ambao bajeti hii tunayoendelea nayo OC ya Mahakama ilipanda kutoka bilioni 60 mpaka bilioni 70, maana yake tunayo nyongeza ya zaidi ya bilioni 11. Kwa hiyo, tuwashukuru kwamba mmetuongezea na sisi tutaendelea kupeleka hizo fedha za OC ili Mahakimu hawa waweze kuhudumia maeneo ambako wanakwenda kuhudumia. Ahsante.(Makofi)

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Supplementary Question 2

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Tarafa ya Ruponda katika Wilaya ya Nachingwea haina Jengo la Mahakama ya Mwanzo; je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Mahakama ya Mwanzo kwenye Tarafa hii ya Ruponda iliyoko Makao Makuu ambayo yako kwenye Kata ya Ruponda? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba sasa nijibu swali Mheshimiwa Amandus Chinguile, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tarafa hii ya Ruponda ambako Mheshimiwa Mbunge ametamka, iko kwenye mpango wetu wa bajeti. Kwenye zile Mahakama 60 tunakwenda kujenga Mheshimiwa Mbunge, na tunafahamu ina umbali wa zaidi ya kilometa 14 kufuata huduma eneo lingine. Kwa hiyo, liko kwenye mpango tumeweka. Ahsante. (Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, Wilayani Rungwe, Kata ya Kiwira ina Mahakama ya Mwanzo. Mahakama hiyo ni ya muda mrefu sana haijafanyiwa ukarabati, ukizingatia Mahakama hiyo inategemewa na Kata ya Ndanto, Isongole, Kinyala, Swaya, Kyimo na Kiwira yenyewe.

Je, ni lini Serikali itakwenda kufanya ukarabati wa Mahakama hiyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Suma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali nilisema kwamba tuna mpango wa kukarabati majengo ya Mahakama kote nchini. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwamba ameridhia wenzetu wa World Bank wametupa zaidi ya dola milioni 90, zaidi ya bilioni 200 kuhakikisha tunaboresha miundombinu ya Mahakama kote nchini. Nikuhaidi Mheshimiwa Mbunge baada ya tafiti yetu kufanyika kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama akishirikiana na Watendaji wa Mikoa kuona maeneo ambapo pamechakaa zaidi tutakuja na mpango huu ili tuingize na hayo maeneo ambayo yamechakaa tuyaboreshe, ahsante. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Majengo ya Mahakama ya Mwanzo katika Jimbo la Mwibara yamechakaa kabisa. Je, ni lini Serikali itajenga upya majengo hayo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimetangulia kusema kwamba fedha hizi ambazo tumezipata haziishi kujenga Mahakama za Mwanzo ni pamoja na za Wilaya, lakini tunajenga pia Integrated Justice Centers kwenye Mikoa, kujenga Mahakama Jumuishi kuanzia Mahakama ya Mwanzo ya Wilaya, Mkoa mpaka ya juu. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mpango huu pia tutakufikia. Ahsante. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Supplementary Question 5

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Wananchi wa Tarafa ya Terati pamoja na Tarafa za jirani ikiwemo Mji mdogo wa Mererani wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za Mahakama. Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo katika eneo hilo? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Regina Qwaray, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Manyara na katika Wilaya ya Simanjiro tunakwenda kujenga Mahakama hiyo ya Terati, lakini siyo hapo tu pia tuna Mahakama ya Orkesumet, Mheshimiwa Regina umekuwa ukilifuatilia hili, tunaanza ujenzi mwaka huu. Ahsante.(Makofi)