Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, kuna mpango gani kujenga mifereji Barabara ya Kigamboni – Kongowe, Mtaa wa Mikwambe, Kata ya Toangoma - Mbagala?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri. Naomba kuuliza, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kuokoa wananchi wa Mikwambe hasa Mtaa wa Zahanati, Rushe, Chambaruba A na B ambao wanaathirika na kutokuwa na mifereji katika barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni upi mkakati wa Serikali wa kujenga mifereji katika barabara zote za lami zilizopo katika Jimbo la Mbagala?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chaurembo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza na la pili Mheshimiwa Chaurembo anaulizia mkakati wa kuhakikisha barabara ambazo tunaweka lami hasa hasa kwenye majiji ni barabara ambazo ni kama barabara za mitaa. Mpango wetu ni upi katika kuhakikisha tunajega mifereji ama mitaro?

Mheshimiwa Spika, Wizara chini ya TANROADS tunayo program ya kuhakikisha barabara ambazo tunaweka lami, tunajenga na mitaro, lakini hata barabara ambazo ni za changarawe pia programu hiyo tunayo.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Mamlaka ya Hali ya Hewa imetabiri mvua kubwa za El-Nino. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na nitumie nafasi hii kutoa maelekezo kwa Meneja Mkuu wa TANROADS kushirikiana na TARURA kuhakikisha barabara za TANROADS ambazo maji yanaenda kwenye barabara za TARURA wakae mara moja hasa hasa kwenye maeneo ya majiji na manispaa kujiandaa na kuhakikisha tunajitayarisha vyema kuhakikisha mvua za El-Nino zitakazonyesha basi mifereji na mitaro tutakuwa tumeitengeneza vizuri ili kuwaepushia wananchi maafa ambayo yanaweza yakatokea kwa mvua kubwa na mifereji kutokuwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, hili la Mheshimiwa Mbunge tumelichukua, lakini nimeona nitoe maelezo ya jumla hasa kwenye majiji na manispaa Mkurugenzi Mtendaji wa TANROADS ajipange na Mkurugenzi Mtendaji wa TARURA ili tuweze kulifanya kwa ufasaha, ahsante sana. (Makofi)