Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani kuhakikisha wazee waliopigana Vita ya Pili ya Dunia chini ya Chama cha TLC wananufaika na mali zao?

Supplementary Question 1

MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu hayo mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mali hizo zenye thamani ya takribani shilingi bilioni 37 ni mali ya Chama cha Wazee Waliopigana Vita ya Pili ya Dunia (TLC) ambazo wana haki nazo pamoja na watoto wao kwa mujibu wa katiba yao. Mali hizo zimekodishwa kwa muda mrefu na pesa zinakusanywa, mfano ni Upanga pamoja na kule Tarime, lakini fedha hizo hazijawafikia wale wazee ambao wanaishi kwa shida na wengine wanafariki hata kwa kukosa chakula: Je, ni lini Serikali itahakikisha fedha hizo zinawafikia wazee hao wafaidike nazo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kamati ya Serikali iliyokaa kwenye majadiliano mbalimbali haijawahusisha wazee hao wala watoto wao: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kupanga siku maalum ambayo atakutana na Kamati ya Wazee na Watoto hao ili washiriki kufikia maamuzi hayo ambayo Serikali imeyafikia?

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kwa ku-declare kwamba baba yangu pia ni mmoja wa veteran waliopigana Vita ya Pili ya Dunia na sasa hivi ana miaka 103, ana akili timamu na anaulizia sana mali hizo.

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, tathmini imeshafanyika na sasa tuko kwenye hatua ya kuhakikisha kwamba tunawafidia wazee hawa. Kwa hiyo, hili linaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tathmini ya kutowahusisha wazee waliopigana vita na watoto wao, tathmini hii ilikuwa pana na ilihusisha taasisi mbalimbali za Serikali. Bahati mbaya viongozi wa Chama cha TLC wote wamefariki, alikuwa amebaki mmoja wakati tathmini inaanza, lakini naye kwa sasa ameshafariki, hata hivyo tulihusisha baadhi ya familia ambazo tuliweza kuzifikia. Kwa hiyo, tathmini iliwahusisha wadau mbalimbali, nafikiri ikiwa nni pamoja na wewe Mheshimiwa Mbunge, tuliweza kupata mawazo yako kwa nyakati mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani kuhakikisha wazee waliopigana Vita ya Pili ya Dunia chini ya Chama cha TLC wananufaika na mali zao?

Supplementary Question 2

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kuna wanajeshi wengi wastaafu waliopigana tokea baada ya uhuru, wamestaafu na mpaka leo wako hai, lakini pensheni zao za mwezi ni ndogo sana: Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwarekebishia ili waweze kukidhi maisha yao? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli wapo watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na wanajeshi wastaafu ambao wamekuwa wakilalamikia pensheni zao kuwa ndogo. Hili ni suala ambalo linafanyiwa kazi kwa pamoja na sekta nyingine zinazohusika na masuala ya pensheni. Kwa hiyo, tutaendelea kuliangalia na kuona ni jinsi gani linaweza kufanyiwa kazi kwa kuzingatia umuhimu wa kazi ambayo wanajeshi hao walifanya na pia kwa kuzingatia uhalisia wa bajeti ya Serikali yetu, ahsante.