Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Je, Tanzania ina Madaktari Bingwa Wazalendo wa magonjwa ya binadamu wangapi na katika magonjwa gani?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya ziada.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Swali langu la kwanza kwa kuwa Madaktari Bingwa 2,098 wako katika sekta ya umma na Madaktari Bingwa 371 wako katika sekta binafsi; je, Serikali inawapatia marupurupu gani Madaktari Bingwa hao ili kulinda ajira zao wasiende sekta binafsi au nje ya nchi? (Makofi)

Swali langu la pili; Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kutambua taaluma bobezi ambazo huwa zinasomewa kwa muda mrefu, waweze kutambua bobezi hizo na kuweka mishahara mikubwa ili kuhamasisha watu waweze kusomea ubobezi huo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake mawili mazuri.

Moja kwanza mpaka sasa kama ambavyo umeona hapa asilimia 75 ya Madaktari wako Serikalini na mpaka sasa Madaktari wengi na watumishi wengi wanapenda zaidi kufanyia kazi Serikalini, maana yake ni kwamba Serikalini kuna uhakika zaidi na incentive nyingi zaidi kuliko kwingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kama unavyojua kwamba Serikali inatoa incentive, mmemsikia Waziri wa Afya akisema kwamba tunatakiwa Madaktari wetu wamekuwa wakikimbia kwenye private sector wakati wa jioni wamekuwa wanafanya kazi, kwa hiyo sasa wameruhusiwa ndani ya hospitali zetu za umma wafanye private clinic humo humo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niweke vizuri pamoja na hayo yote ambayo Serikali inafanya bado tunafikiri tunahitaji wawe umma lakini pia wawe private sector, kwa hiyo pande zote mbili Madaktari wetu tungefurahi wakafanya kazi sehemu zote, wawe private sector wengine wawe public sector. Tungefurahi wafanye kote kwa sababu kote wanamhudumia Mtanzania yuleyule.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni Je, Serikali inafanya nini kwa wale wanaosoma muda mrefu. Mheshimiwa Waziri wa Afya alipeleka hilo tatizo kwa Mheshimiwa Rais wetu. Mheshimiwa Rais wetu na ameshatoa maelekezo tukae na utumishi ili kujadili kuona Madaktari ambao wanasoma muda mrefu ni kwa namna gani utumishi wakaweka incentive au kuongeza mshahara kulingana na ule muda wanaosoma ili wengi wavutiwe kusoma masomo hayo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais wetu ameshatoa maelekeo ya kutatua tatizo hilo. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Je, Tanzania ina Madaktari Bingwa Wazalendo wa magonjwa ya binadamu wangapi na katika magonjwa gani?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu gani unafanyika kuwapeleka Madaktari Bingwa kama wakiwa wamehamishwa, kwa sababu Mkoa wetu wa Iringa sasa ni karibu mwaka wa tatu Daktari Bingwa wa Mifupa amehamishwa na hatujampata na kuna ajali nyingi sana. Je, ni lini sasa tutampata katika hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nalichikua tatizo lake kama alivyolisema kuona tunalishughulikiaje, lakini jana Mheshimiwa Waziri wa Afya ameelekeza Idara ya Utumishi wakishirikiana na Idara yetu ta IT na kuwasiliana na Utumishi ili tuwe tunaweza kuona kwenye mfumo jinsi ambavyo watumishi wa afya wamegawanyika maeneo mbalimbali na hiyo itaturahisishia kuona ni namna gani, maeneo gani ambayo yana upungufu, ni maeneo gani wamezidi watumishi kwa namna hiyo tutakuwa tunapanga kwa kujua vizuri wamezidi wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nakubaliana na wewe kwamba Madaktari Bingwa wengi wako Dar es Salaam, wako kwenye Miji mikubwa na Waziri ameshatoa maelekezo kuona namna gani iyo Mikoa ya mbali wanapelekwa hao Madaktari Bingwa. (Makofi)