Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Simbo hadi Ilagala?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Daraja la Malagarasi Lower litakuwa na kilometa saba za lami. Je, Serikali haioni haja ya kufanya upembuzi yakinifu haraka wa kipande hiki kidogo cha Simbo - Ilagala chenye kilomita 40? Ahsante.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Nashon, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Mheshimiwa Mbunge nimeisikia na Mheshimiwa Mbunge naomba unipe muda ili niweze kufuatilia kipande cha barabara hii ili tuweze kuona lile ambalo linawezekana. Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha mitandao yote ya barababara ambayo ipo chini ya TANROADS, kwanza zile ambazo hatujafanya upembuzi yakinifu, tunafanya upembuzi yakinifu na kuwa na database ili fedha zinapopatikana tu ujenzi wa barabara hizi unaanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua pia mahitaji ni mengi ya barabara kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini naomba Waheshimiwa Wabunge wanipe muda, nitakaa na timu yangu ya Wizara lakini kwa kushirikiana na Kamati yetu ya Miundombinu ya Bunge, tuangalie mahitaji haya makubwa na majira haya tunayoingia ambayo Waheshimiwa Wabunge wanafahamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeahidi vingi kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanya kila aina ya jitihada fedha zinapatikana, kazi inaenda vizuri, lakini hata mahitaji ambayo bado tutaangalia namna ya kujipanga tukisaidiwa na Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati, kaka yangu Kakoso, Makamu Mwenyekiti Mama Anna Kilango, tuangalie resources ambazo zinapatikana ndani ya Serikali. Tufanyaje kwa kushirikiana na Waheshimiwa Wabunge ili yale ambayo tuliwaahidi wananchi tuweze kuyatekeleza kwa kiasi kikubwa kadri inavyowezekana. (Makofi)