Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, lini jengo jipya la X-Ray litajengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kwamba mkopo unaotolewa na NHIF ni wa shilingi milioni 200 na utaifanya hospitali yetu kulipa kiasi cha shilingi milioni 6,500,092 kwa mwezi, katika miezi 36, na itakuwa imelipa jumla ya shilingi milioni 237, pamoja na riba ya asilimia 11.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haioni nia njema ya Wilaya ya Maswa ya kukopa NHIF kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la X–Ray ili Serikali itoe fedha ambayo si mkopo kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo la X–Ray na wananchi wapate huduma?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini Serikali vilevile itajenga Kituo cha Afya cha Kata ya Sangamwalugesha katika Kijiji cha Sangamwalugesha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyongo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya inatumia fedha za Serikali Kuu na fedha zinazotokana na makusanyo ya ndani, zikiwemo fedha za uchangiaji wa huduma za afya lakini pia na za Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze sana Halmashauri ya Maswa na nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge; kwa sababu yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii na amekuwa mfano mzuri kuonesha tunaweza tukatumia fursa za mikopo ya NHIF, tukaboresha miundombinu na hatimaye tukatoa huduma bora zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie pamoja na kwamba tutakatwa shilingi milioni 6,500,000, bado watakuwa na uwezo wa kuendelea kujiendesha. Pia, jengo litakalojengwa litaongeza mapato ya Hospitali yetu hii ya Maswa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili kuhusiana na hiki kituo cha afya, naomba tulipokee tukafanyie tathmini, tuone kama kinafiti kwenye vituo vya afya vya kimkakati ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya. Ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, lini jengo jipya la X-Ray litajengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa?

Supplementary Question 2

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mahitaji ya jengo la X–Ray katika Wilaya ya Maswa, linafanana kabisa na Kituo cha Afya cha Upuge. Kuna mitambo pale kwa miaka mitano ipo kwenye mabox, X–Ray Mashine na Ultrasound. Lini Serikali itajenga jengo? Kwa sababu mitambo hii itaoza, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kwanza kumuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI; kwamba Serikali ilishapeleka mashine ya X–Ray, ilishapeleka Ultrasound, na wao kupitia mapato ya ndani wana uwezo wa kujenga jengo la X–Ray na Ultrasound ili wananchi waanze kupata huduma hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wajibu wao, na nitoe wito, kwamba wanatakiwa kuweka kwenye bajeti haraka iwezekanavyo, na ikiwezekana kwenye mapitio ya bajeti mwezi Desemba wananchi waanze kupata huduma za X-Ray na Ultrasound. Ahsante.