Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR aliuliza: - Je, ni kwa kiwango gani bahari zinachangia kukua kwa uchumi kupitia uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana pia nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wa sekta hii ya uvuvi kwenye Pato la Taifa kwa kiwango cha asilimia 1.8, tunakubaliana kwamba mchango huu bado ni mdogo sana, lakini nafahamu kwamba ipo mipango ya Serikali kununua meli kwa ajili ya uvuvi wa Bahari Kuu. Nataka kufahamu ni stage gani tumefikia kwenye uagizaji wa meli hizi kwenda kuvua kwenye Bahari Kuu?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nataka kujua ni kwa namna gani mipango hii ya Serikali kwenye Wizara hii ya Uvuvi inaishirikisha Zanzibar katika kukuza Uchumi wa Bluu? Ahsante.

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Bakar Hamad Bakar. Swali lake la kwanza anataka kujua kuhusu mchango.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mchango huu ni mdogo, mchango wa asilimia 1.9 ni mchango mdogo na ndiyo maana Serikali imekuja na mikakati mbalimbali ambayo itakuja kusaidia sana kuinua kipato hiki. Moja ya mikakati ambayo Serikali imekuja nayo ni pamoja na ujenzi wa Bandari ya Uvuvi. Tunakwenda kujenga Bandari ya Uvuvi pia kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchakata mazao ya samaki, pia kufufua viwanda ambavyo tayari vimeshakufa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba asilimia 1.9 ni asilimia ndogo na Serikali iko na mkakati wa kufanya kazi hiyo ikiwa ni pamoja na kufufua Shirika la TAFICO ambalo tayari limeshakufa. Kwa hiyo, tunayo mikakati kama Serikali kwamba mikakati hiyo ambayo tumeiweka tukiitimiza vizuri tunaweza tukaongeza pato kutoka 1.9 kwenda juu zaidi. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute subira kwamba iko mikakati Serikali inajipanga kwa ajili ya kwenda kuimarisha jambo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ametaka kujua ni lini ununuzi wa meli hiyo utakamilika. Mchakato wa ununuzi wa meli upo unaendelea lakini umesimama kidogo kwa sababu za kibajeti. Kwa hiyo, mara Serikali itakapopata fedha ununuzi wa meli hiyo utaweza kufanyika mara moja. Ahsante.