Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:- Je, ni mafunzo ya aina gani yanatolewa kwa vijana wa Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nachukua nafasi hii kuipongeza Wizara kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya kwa vijana nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; je, Wizara mnampango gani au mnafanya utafiti kuona mafunzo haya jinsi gani yanawanufaisha vijana hao mara baada ya kumaliza mafunzo hayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; nataka kujua kama Wizara mnamkakati gani sasa wa kuweza kuwaongezea au kuwapa mitaji mikubwa zaidi kwa vile vikundi ambavyo vinafanya vizuri zaidi ili kuweza kuzalisha bora zaidi na kuzalisha vitu vizuri zaidi ili kuendelea kujiajiri na kuajiriwa ili kuweza kuongeza mapato kwa nchi yetu?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Latifa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunao mpango wa ufuatiliaji na tathmini ambao kila baada ya miezi mitatu tunafanya kupita kwenye maeneo ambayo vijana hawa wapo wakipata mafunzo lakini pia wale ambao wanapewa mitaji mbalimbali. Tumekuwa na utaratibu wa kufanya ufuatiliaji na tathmini ili kubaini na kuona kama kuna tija katika fedha ya nyingi ya Serikali ambayo inatolewa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweza kuwawezesha vijana kujikimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwenye hatua ya pili ambapo ameniuliza swali kama tunawapa mitaji? Ni kweli kwamba vijana hawa hatuwaachi tu kwa maana ya kuwatambua na kuwapeleka kwenye maeneo yao ya kupata mafunzo na wanapomaliza kupata mafunzo tunawaunganisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, wapo ambao tunawapeleka VETA, wapo amabao tunawaunganisha kama wamefuzu vizuri kwenda kwenye maeneo ya ajira. Lakini pia tunwaratibu na kuwasaidia kuweza kupata ile mikopo ya 10% ya halmashauri ambapo mwongozo kwa sasa nikijibu swali la kwamba tuwape mitaji inayojitosheleza, tilikua tunatoa kwa vikundi vya watu 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hatua ya sasa na kwa Mwongozo mpya na kwa usikivu wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa vijana aliona ni vema aweze kubadilisha badala ya kuwapa vijana 10, sasa tunatoa mkopo kwa kuanzia shilingi milioni moja mpaka shilingi milioni 10 tumetoka sasa shilingi milioni 10 mpaka shilingi milioni 50 kwa kijana mmoja mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia hatua nyingine tunawasaidia pia kuweza kupata mikopo kupitia benki. Zipo benki ambazo zimekwisha kuanza kuonesha mfano. Benki a Azania inatoa mikopo kwa single digit kwa sasa lakini zaidi ya hapo pia tunayo mifuko mingine, katika Wizara ya Kilimo tunao Mfuko wa Pembejeo za Kilimo ambapo vijana hawa nao pia wakimaliza kwenye mafunzo mbalimbali iwe VETA au kule kwenye programu za unenepeshaji ng’ombe au BBT tunawaendeleza kwenda mbali zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni ninayo furaha kukwambia tumepeleka vijana tena awamu nyigine ambao watafikia sasa 700 wanaoenda kupata mafunzo nchini Israel ili kuweza kuwatengeneza vijana na kuweza kuhakikisha kwamba kwa kweli wanatumia fursa za kiuchumi na kushiriki ujenzi wa Taifa lao, ahsante.