Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, lini TANESCO watalipa fidia kwa wananchi wa Rorya waliopisha eneo la kupitisha umeme mkubwa toka mwaka 2011?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pia nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye matumaini kwa wananchi wangu wa Rorya, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa kuwa Sheria ya Uthamini inatamka wazi kwamba thamani ya ardhi inapaswa kulipwa ndani ya miezi sita, lakini wananchi hawa wamedai malipo yao toka mwaka 2011 na hawajalipwa. Nataka nipate commitment ya Serikali itakapofika Novemba kama wananchi hawa hawajalipwa uthamini wa ardhi yao, je, Serikali itakuwa tayari sasa kurudia uthamini kwa mujibu wa Sheria inavyotamka kwamba wananchi wale walipwe ardhi kwa mujibu wa Sheria inavyotamka?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa jambo hili limekuwa ni la muda mrefu toka mwaka 2011 na sasa liko ndani ya Ofisi ya Mkurugenzi nataka nipate commitment ya Serikali hasa Ofisi ya Wizara ya TAMISEMI, je, ni lini watalipa fedha ili wathamini warudi site wakamilishe uthamini na upande wa TANESCO waweze kulipa fidia kwa wananchi hawa?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jafari Chege, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu kurudia zoezi ikifika Novemba, zoezi hili limeshachukua muda mrefu nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali imeshatenga fedha kiasi cha milioni 350 ili wananchi 231 wanaodai fidia walipwe ikifikia Novemba, 2023. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi hili tunaenda kulikamilisha na kwa sababu limechukua muda tutafuatilia kwa ukaribu kuhakikisha kwamba linakamilika.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili kuhusiana na kutoa fedha, tayari Serikali kupitia TANESCO imeshatoa fedha kiasi cha shilingi milioni 15 kwa ajili ya kukamilisha zoezi la uthamini. Tutafuatilia kuhakikisha kwamba Halmashauri ya Rorya inakamilisha taratibu hizi kwa wakati ili zoezi hili liweze kukamilika kwa wakati kwa kadri ambavyo imepangwa, ahsante. (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba nitumie nafasi hii tena kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rorya kuhakikisha kwamba fedha hizi ambazo wenzetu wa TANESCO wameshazipeleka kwenye halmashauri ile ziweze kutumika mara moja na kulipa fida hiyo. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, lini TANESCO watalipa fidia kwa wananchi wa Rorya waliopisha eneo la kupitisha umeme mkubwa toka mwaka 2011?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mradi wa Geita - Nyakanazi na Nyakanazi - Rusumo kuna baadhi ya wananchi wa Biharamulo ambao wanapitiwa na mradi ule katika Kata nne za Rusahunga, Kaninha na Nyakahula nao pia bado hawajalipwa pesa zao za fidia. Je, ni lini Serikali itaweza kukamilisha malipo hayo kwa baadhi ya watu ambao walikuwa hajalipwa pesa zao? Ahsante sana.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali ya Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na fidia ya Geita - Nyakanazi tayari Serikali ilishatenga fedha bilioni sita na tayari fedha bilioni 5.9 zilishalipwa kwa ajili ya wananchi na wananchi waliobakia ni wananchi 49 tu, tunaamini taratibu zikikamilika na wao wataweza kulipwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Nyakanazi -Rusumo pia Serikali ilishatenga fedha bilioni 3.8 na tayari bilioni tatu ilishalipwa, wananchi waliobakia ni 39 tu. Nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia na kwa sababu fidia hii imekamilika kwa zaidi ya asilimia 95, tutafuatilia kuhakikisha kwamba kidogo kilichobakia kinaweza kukamilika, ahsante sana. (Makofi)