Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanzisha Mamlaka ya Kuratibu na Kupambana na Magonjwa Yasiyoambukiza?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa tafiti zinaonyesha magonjwa yasiyoambukizwa yanakua kila siku; je, Serikali haioni haja sasa ya kuanzisha mchakato wa kuanzisha Mamlaka ya Kusimamia Magonjwa Yasiyoambukizwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni tuna Hospitali ya Kilimatinde inayoendeshwa kwa ubia kati ya Serikali na Kanisa la Anglikana, lakini hospitali hii haifanyi vizuri; je, nini mkakati wa Serikali wa kuiboresha hospitali hii iweze kusaidia katika kupambana na magonjwa yasiyoambukiza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza la kwamba magonjwa haya ya kuambukizwa yanaongezeka, ni kweli yanaongeza na hasa Kusini mwa Afrika yanaongezeka sana. Sasa hata ukiangalia leo kwenye UKIMWI, wewe ni shahidi tunatoka kwenye suala la kuuangalia UKIMWI peke yake kama UKIMWI, lakini tunaangalia magonjwa kwa ujumla na data zinaonyesha kwamba unapomchukua mgonjwa wa matatizo ya UKIMWI ukaangalia suala la pressure wakati huohuo sukari na ukatibu yote kwa pamoja, matokeo yanakuwa mazuri kuliko unapotibu ugonjwa mmoja na kumwangalia kama ugonjwa mmoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nafikiri pamoja pia na kuanzisha Taasisi kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge ambayo itashughulikia hilo moja, tunaweza tukatumia fedha nyingi ambazo bora tu hizo fedha tungepeleka kuenga vituo vya afya kule kwenye jimbo lako.

Kwa hiyo, nafikiri Mheshimiwa Mbunge aendelee kukubaliana na Serikali kwa namna hii ambayo itatumia rasilimali vizuri, lakini wakati huo huo mgonjwa huyo akaangaliwa kwa ujumla wake, kwa sababu mgonjwa anapokuja huwezi tu kusema ni mgonjwa wa pressure au mgonjwa sukari unamwangalia kwa ujumla wake kuanzia saikolojia na mambo mengine ambayo yanafuatana na hilo. Kwa hiyo tukiyaangalia kwa pamoja namna hiyo tutapata matokeo mazuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili la hospitali hiyo ambayo Serikali iko pamoja na Kanisa. Mheshimiwa Mbunge mwenyewe ni shahidi kwenye hii hospitali kwamba Serikali imepeleka watumishi, lakini vilevile Serikali inatoa dawa, pia wanapewa ile asilimia ya basket fund kwa maana ya kuboresha mambo yao. Sasa ninachofikiri kama Serikali imefanya yote hayo na bado Mheshimiwa Mbunge kama mwakilishi wa wananchi bado wananchi wake wanalalamika kwamba huduma inayotolewa bado ni ya chini maana yake inawezekana kuna suala sasa la kiutawala.

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge, Manyoni Mashariki ni karibu hapa, saa nne zinatutosha mimi na yeye twende site, tukae kwa saa nne tuangalie mambo mengi ili tuweze kuhukumu kwa haki na kutoa maamuzi ya kuboresha hiyo hospitali kwa namna ambayo tutakuwa tuko site, ahsante.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanzisha Mamlaka ya Kuratibu na Kupambana na Magonjwa Yasiyoambukiza?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa Serikali ina mapango wa kitaifa wa kupambana na haya magonjwa yasiyoambukizwa; je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha sasa tunashuka chini sasa kwenye ngazi ya Kata na Vijiji ambako kuna uhitaji mkubwa ili hawa wananchi waweze kufikiwa na huduma hizo? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, moja ya mkakati ni kuwa Serikali inaendelea kutoa hamasa kuhusu magonjwa haya na mmekuwa mkiona kwenye tv zetu. Pia kama ambavyo tumesema hapa Wizara ya Afya inatengeneza miongozo na mojawapo ya miongozo kwenye eneo la dawa, kwenye eneo la kutoa elimu na eneo la tiba. Kwa hiyo, tutaanza kushuka mpaka level ya zahanati na kwa mwaka huu tunaenda kusajili hawa watu wa afya jamii ambao watafanya hiyo kazi kwenye kufika kwenye vitongoji vyetu. Kwa hiyo ni wazo zuri na tunakwenda kutekeleza kwa nmna hiyo.