Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwanza ili kuweka kumbukumbu sawa naomba nirekebishe jina langu kama lilivyotajwa na Mheshimiwa Waziri, mimi ninaitwa Mheshimiwa Kasalali na sio Kasasali.

Mheshimiwa Spika, baada ya marekebisho hayo, naomba niishukuru Serikali kwa majibu mazuri na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa utayari wake alipokuja kwenye Jimbo la Sumve kusikiliza changamoto zetu.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza, kwa kuwa kumeibuka aina mpya ya kangomba katika sekta ya mawasiliano ambapo kampuni za simu mara baada ya kufanya utafiti wa maeneo ambayo wataweka minara wamekuwa wakishirikiana na wajanja wachache wanaokwenda kuyatwaa maeneo haya kwa kuwalaghai wamiliki na hatimaye wao kuingia kwenye orodha ya watu wanaopangishwa na minara hiyo ya simu.

Je, nini tamko la Serikali juu ya ulaghai huu ambao umekuwa ukifanywa kupitia makampuni ya simu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Kata za Wala, Mwabomba na Maligisu hali ya mawasiliano ni mbaya sana na Serikali imesema inao mpango wa kupeleka mawasiliano katika maeneo hayo. Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kupeleka mawasiliano haraka sana katika kata hizo ili kurahisisha mawasiliano kwa watu hawa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kuomba radhi kwa kukosea jina la Mheshimiwa Mbunge. Napenda sasa kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni Mbunge wa Sumve kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kama ambavyo nimejibu katika majibu yangu ya msingi, kuna maeneo ndani ya jimbo hili bado kuna changamoto na ndio maana Serikali tunaenda kufanya tathmini ili tujiridhishe ni hatua gani ambazo tunazichukua aidha kama ni kujenga mnara au kuongeza nguvu. Lengo ni kwamba mawasiliano ndani ya Jimbo hilo la Sumve yaweze kuimarishwa.

Mheshimiwa Spika, kwa swali la ulaghai. Nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge, lakini kwa picha ambayo nimeiona nikiwa nafanya ziara. Kumekuwa na maeneo ambayo yamekuwa na changamoto kweli, watoa huduma kuhusishwa na jambo kama hili.

Mheshimiwa Spika, lazima nikiri kwamba sina uhakika na uthibitisho wa namna ambavyo watoa huduma wanashiriki, isipokuwa naamini kwamba kuna wajanja ambao wanahisi kwamba eneo fulani linakwenda kujengwa mnara basi wao wanawahi kwenda kulinunua ili baadaye wao ndio waweze kulipwa.

Mheshimiwa Spika, pia ninaamini kwamba kwa kushirikiana na Ofisi ya Halmashauri kwa sababu tulishatoa maelekezo, ujenzi wa minara ni lazima Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ihusishwe katika hatua zote ili kuhakikisha kwamba tumeondokana na migogoro ambayo inaweza ikatokea kwa sababu ya ujenzi wa minara.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia fursa hii. Nina swali la nyongeza. Jimbo la Newala vijijini maeneo yake mengi yanakosa mawasiliano ya simu. Je, ni lini Serikali itakuja kujenga minara katika jimbo lile ili mawasiliano yaweze kuboreshwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa bahati nzuri, mimi pamoja na Mheshimiwa Mbunge tumeshafanya ziara katika jimbo lake na maeneo ambayo yalikuwa na changamoto, Serikali iliyachukua na tayari yameingizwa kwenye utekelezaji wa miradi 758 ambapo kata 713 zinaenda kuguswa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi bali awe na subira wakati utekelezaji ukiwa unaanza, ahsante sana.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Kata za Masanga na Ngofia katika Jimbo la Kishapu hazina mawasiliano kabisa ya simu. Je, ni lini Serikali itapeleka minara katika kata hizo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kati ya majimbo ambayo yamepata minara mingi sana, minara zaidi ya tisa ni katika Jimbo la Kishapu na utekelezaji wake uko katika hatua mbalimbali na umeshaanza. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge aendelee kushirikiana na watoa huduma ili miradi hii ikamilike kwa wakati, ahsante sana.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 4

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itatatua tatizo la mawasiliano katika Kata ya Mchuki pamoja na Mbuchi kwenye Jimbo la Kibiti?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Kibiti kuna maeneo ambayo yana changamoto ya mawasiliano. Vilevile kuna maeneo ambayo tayari Serikali imeyaingiza katika ile miradi 758. Kama kuna maeneo ambayo yatabaki kuwa na changamoto Serikali inayapokea ili iwatume wataalam wake wakafanye tathmini na tujiridhishe ukubwa wa matatizo yaliyopo pale then tupate fursa ya kupeleka huduma ya mawasiliano, ahsante.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 5

MHE. NASHONI W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali. Ni lini itapeleka mawasiliano katika Kijiji cha Songambele, Kalilani, Mkanga pamoja na Chagu? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niwatoe wasiwasi Waheshimiwa Wabunge wote. Miradi ya Mawasiliano ambayo tumesaini mwezi wa tano iko katika hatua za awali za utekelezaji wake. Ninaamini kabisa kwamba kwa sababu Waheshimiwa Wabunge hawajaanza kuona minara ikiwa ina simama katika maeneo yao, wavute subira ili tutakapoanza utekelezaji wake na baadaye minara itakapoanza kuonekana basi tutaweza kubaini maeneo ambayo yatakuwa bado yanahitaji kupelekewa mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Songambele, tayari imeingizwa katika vijiji 2116 ambavyo vinafanyiwa tathmini na tayari Serikali imeshaanza kutafuta fedha ambapo Mheshimiwa Rais alishapata fedha ya kufikisha minara 600 mingine. Ninaamini Mheshimiwa Mbunge, atakuwa mmoja wa wanufaika katika minara hiyo 600, ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 6

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kumekuwa na changamoto kubwa sana ya mawasiliano katika Kata ya Makanya, Mbwei na Maibwi; je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika Kata hizo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari tulishawasiliana na Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi na amekuwa akinijulisha kuhusu changamoto hiyo. Maeneo na kata ambazo zina changamoto hizo tayari Serikali imeshazipokea na imeziingiza kwenye mpango wa utekelezaji wa miradi ambayo inakuja kadri ya upatikanaji wa fedha utakavyoruhusu, ahsante sana.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 7

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Ipande Kijiji cha Mhanga, Kata ya Sanjalanda Kijiji cha Gurungu, Kata ya Mgandu Kijiji cha Itagata na Kata ya Wamagande Kijiji cha Kitanura hakuna mawasiliano kabisa. Nini kauli ya Serikali kuwapelekea wananchi hawa minara ya mawasiliano ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania ya sasa ni Tanzania ya Kidigitali, hatutahitaji mtanzania yeyote aachwe nyuma, kwa hiyo naomba nipokee changamoto hizi ili tupeleke wataalam wakaangalie ukubwa wa tatizo ili tupeleke huduma ya mawasiliano na watanzania wote washiriki katika uchumi wa kidigitali, ahsante sana.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha tatizo la kutokuwepo mawasiliano ya simu ya uhakika katika maeneo mengi ya Jimbo la Sumve linatatuliwa?

Supplementary Question 8

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Serikali iliahidi kujenga minara ya mawasiliano kwenye Kata ya Bugarama na Kata ya Kibogora lakini kazi haijaanza hadi sasa. Ni lini Serikali itakuja Ngara kwenye Kata hizo kujenga minara ya mawasiliano? Ahsante sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwenyewe na Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro tulishatembelea jimbo lake na tulizunguka katika maeneo yote ambayo yana changamoto ya mawasiliano na baada ya kugundua changamoto hiyo Serikali ikaingiza katika mpango wa utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, katika mpango huo wa utekelezaji, tayari watoa huduma wameshapatikana lakini utoaji wa huduma hii una mchakato kidogo unaposaini, lakini kuna masuala ya vibali kwenda kupata ardhi kuingia mikataba na wenye ardhi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo haya kwa kuwa Serikali imeshaahidi hakuna eneo ambalo litaachwa bila kujengwa mnara, ahsante sana.