Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru na nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa miradi mingi inayotekelezwa na TARURA, kumekuwa na changamoto ya ubora wa wakandarasi wanaotekeleza miradi hii.

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha katika miradi hii, pamoja na Serikali kutenga pesa nyingi lakini wakandarasi wanaopatikana wawe na ubora wa kuhakikisha barabara zile zinakuwa vizuri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwenye Jimbo la Ukerewe barabara inayounganisha Kata ya Nkilinzya na Kata ya Bukindo kuna daraja pale linaleta shida kubwa sana. Je, ni lini Serikali itatusaidia kupata pesa za kujenga daraja linalounganisha Kata ya Bukindo na Kata ya Nkilizya? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kusisitiza kwa Mameneja wote wa TARURA wa Mikoa na Wilaya, kwamba Serikali ilikwishatoa maelekezo kwamba kila tunapotekeleza miradi ya Barabara, kwanza lazima tupate wakandarasi wenye sifa na uwezo wa kujenga barabara kwa kuzingatia ubora na thamani ya fedha, lakini kukamilisha kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, pili, tulishaelekeza kuchukua hatua kwa wakati kwa wakandarasi ambao wataonesha kutokuwa na uwezo mzuri wa kujenga barabara hizo. Pia, kuhakikisha kwamba ikiwezekana tunavunja mikataba hiyo kwa kufuata taratibu za kisheria na kupata wakandarasi ambao wana sifa hiyo. Kwa hiyo, naomba nisisitize kwenye eneo hili, kwamba ni wajibu wa Mameneja wa Mikoa, pia wa Wilaya lakini na halmashauri zetu na Mabaraza ya Madiwani kuhakikisha kwamba wanajiridhisha na ubora wa barabara kabla mradi haujakamilika.

Mheshimiwa Spika, pili, kuhusiana na daraja linalounganisha Kata ya Bukindo na Nkilizya ambalo liko katika halmashauri ya Ukerewe, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunahitaji kufanya tathmini na hivyo meneja wa TARURA Wilaya afanye tathmini, watuletee gharama. Tutaona kama Serikali Kuu inahitaji kutoa fedha ama mapato ya ndani yanaweza kujenga daraja hilo, ahsante.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Daraja la Makulu Villa ni daraja linalounganisha Wilaya ya Simanjiro na Wilaya ya Same, lakini daraja hili limekuwa na changamoto kubwa kwa kuwa wakulima na wafugaji wanashindwa kufanya biashara zao. Je, Serikali imejipanga vipi katika kujenga daraja hili ili kuwasaidia wananchi hawa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kuhusu Daraja la Makulu Villa ambalo linaunganisha Halmashauri ya Simanjiro na Same kwamba ni changamoto na linakwamisha shughuli za kiuchumi kwa wananchi, wakulima na wafugaji, naomba Serikali tulichukue hili na tutafanya tathmini kuona uwezekano wa kuweka mpango kwa ajili ya ujenzi au ukarabati wa daraja hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, barabara za milimani zinapowekewa kifusi, mvua inavyonyesha kifusi kinazolewa kwa hiyo Serikali inapoteza fedha nyingi sana. Je, ni lini Serikali itaweka zege katika barabara ya Chome – Tae na Yavumali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara za milimani kwa kweli tukizijenga kwa kifusi mara nyingi baada ya msimu wa mvua barabara zinaharibika kabisa na hivyo thamani ya fedha inapotea na ndiyo maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia TARURA tumefanya tathmini ya aina ya barabara kulingana na hali ya kijiografia ya maeneo husika ikiwemo Halmashauri ya Same, ambayo ina milima mingi.

Mheshimiwa Spika, moja ya solution ambayo tumeitafuta, ni kuanza kujenga barabara hizo kwa kutumia mawe. Kwa sababu mara nyingi maeneo yenye miinuko yana mawe pia, lakini pili kutumia zege. Kwa hiyo, kwa hizi barabara ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, naomba tuzichukue, tufanye tathmini, halafu tuone uwezekano wa kujenga kwa kiwango cha changarawe, ahsante. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Mji wa Bunda ni mji unaokua. Serikali iliahidi kujenga barabara za mitaa kwa kiwango cha lami; je, ni lini sasa Serikali itahakikisha inajenga kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, barabara za lami katika Halmashauri ya Mji wa Bunda ni jambo la msingi na Serikali ilishaahidi na imeshaanza utekelezaji kwa awamu. Najua kuna barabara za lami pale zinaunganisha mitaa, lakini nafahamu kwamba kuna uhitaji mkubwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuhakikisha kwamba tunajenga barabara za lami kwa kadri ya mahitaji ya Mji wa Bunda, ahsante sana. (Makofi)

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi. Mji wa Mtwango, Jimbo la Lupembe ni eneo ambalo linakua kwa kasi sana. Serikali ina mpango gani wa kujenga lami katika eneo la Mtwango na barabara ya kwenda Ikuna? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika naomba kujibu swali la uhitaji wa barabara ya lami katika Mji wa Mtwango ambao unaunganisha Ikuna na Mtwango.

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mji wa Mtwango unakua kwa haraka sana lakini tulishaelekeza Meneja wa TARURA kuweka vipaumbele vya ujenzi wa barabara za lami, katika Halmashauri zetu zote katika zile fedha za Bajeti za TARURA tulielekeza kwamba angalau kuwe na kipaumbele cha kuanza ujenzi wa barabara za lami.

Mheshimiwa Spika, naomba nisisitize kwamba Meneja wa TARURA Wilaya ya Njombe asimamie maelekezo hayo, lakini kama fedha ile ya bajeti haitoshelezi afanye tathmini na kuleta Ofisi ya Rais, TAMISEMI tuweze kuona uwezekano wa kupata fedha zingine kwa ajili ya kuongeza nguvu ya utekelezaji wa mradi huo, ahsante sana. (Makofi)

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Ilula kwenda Image - Igumu ipo katika mpango wa kujengwa lami kupitia mradi wa RISE. Je, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa ili wananchi wapate barabara bora, kwa sababu barabara hiyo sasa hivi ipo katika hali mbaya sana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Mpango wa RISE unaendelea kutekelezwa, ni kweli kwamba barabara hii ya Ilula - Image na Igumu ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge ziko kwenye mpango huu wa RISE, nimhakikishie kwamba mpango ule unaendelea kutekelezwa na muda utakapofika tutahakikisha kwamba barabara hizo kwa kadri tulivyojipangia mpangokazi, zinatekelezwa kwa kiwango hicho ambacho kimepangwa kwenye mpango wetu. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, barabara ya Himo - Sokoni kwenda Lotima ina kilometa 7.5 na Mheshimiwa Waziri Mkuu aliagiza kwamba TARURA waweze kuijenga kwa kiwango cha lami na mmeanza mmejenga mita 800 tu.

Je, mnatoa kauli gani kuhusu kumalizia barabara hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba ni kweli maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Serikali imekwishaanza kutekeleza kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, tumeanza na mita 800 lakini tunafahamu barabara ile ina urefu wa kilometa 7.5 tutakwenda kwa awamu, safari ni hatua tumeanza, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kuweka kipaumbele kuhakikisha kilometa hizo 7.5 zinajengwa kiwango cha lami, ahsante.