Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, Serikali haioni kuwa kufutwa kwa Form 2c katika huduma ya Bima ya Afya inakosesha mgonjwa kupata dawa iliyokosekana hospitali aliyotibiwa?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa maelezo mazuri ya Serikali na niipongeze Serikali kwa kweli dawa zipo kwenye vituo vyetu na wananchi wanapata dawa. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ni nini mkakati madhubuti wa Serikali kuhakikisha kuwa dawa hizi zinazopatikana sasa hivi ziendelee kupatikana katika vituo vya afya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tupate ufafanuzi wa utaratibu uliowekwa pale mgonjwa anapokosa dawa katika hospitali na duka linalomilikiwa na hospitali ili sasa apate dawa kwa ajili ya tiba inayohusiana na matibabu yake, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT FESTO J. DUGANGE) K.n.y. WAZIRI WA AFYA: Mhehimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mkakati wa kuhakikisha kwamba baadhi ya dawa ambazo zinakosekana zinapatikana, moja, tumeelekeza na kusisitiza vituo vyote vya Serikali vifungue maduka ya dawa. Mbali na dispensing za hospitali zenyewe lakini wafungue maduka ya dawa ndani ya hospitali zenyewe, na wahakikishe yale maduka yana dawa zote zilizopo katika ngazi ya kituo husika; ili mgonjwa akikosa dawa pale dispensing aweze kuwa-referred ndani ya hospitali kwenda kuchukua dawa kwenye duka la dawa la hospitali. Kwenye mkakati huo tumeweka kwamba dawa zote lazima zipatikane kwenye duka, ikiwa ni alternative ya filling kutoka dispensing.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, utaratibu ni kwamba mara mgonjwa akiandikiwa cheti cha dawa na kwenda dirisha la dawa kupata dawa zile akapata chache na moja kakosa anaandikiwa cheti kidogo kwa ajili ya kwenda kwenye duka la dawa na kupata dawa zile; na tutaendelea kusimamia utaratibu huo.