Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN. MWINYI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga ofisi ya NIDA katika wilaya ya Mkoani?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED ABDULRAHAMAN. MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Ofisi ya NIDA ya Wilaya ya Mkoani ni kichumba kidogo sana ambacho akiingia mteja mmoja wengine wanabakia nje wanapigwa na mvua, wanapigwa na jua…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa swali.

MHE. MOHAMED ABDULRAHAMAN. MWINYI: Je, Serikali haioni haja ya kuwatafutia jengo jingine kuondoa adha hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa kuna wananchi ambao wamejisajili mwaka 2018, 2019, 2020 mpaka leo hawajapata vitambulisho vya NIDA na wanaojisajili sasa hivi wanapata vitambulisho vya NIDA; je, nini kauli ya Serikali? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuwatafutia jengo lingine kwa kweli tunatambua kwamba zipo wilaya zenye changamoto ndiyo maana tumesema zitaendelea kujengewa ofisi baada ya hizi 31 zitakazofanyika kwenye mwaka wa bajeti ujayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kwa hali ambayo ameieleza Mheshimiwa Mbunge niombe uongozi wa Wilaya ya Mkoani kule Mwinyi Pemba waone uwezekano wa kuwatafutia, kwa sababu wananchi wanaosajiliwa ni wananchi walewale walio chini ya Mkuu wa Wilaya, chini ya mamlaka zao za serikali za mitaa. Lakini nimuahidi pia tutatembelea huko baada ya bajeti hii ili kuona namna ya kutatua hilo tatizo alilolisema.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu wananchi waliojisajili muda mrefu na hawajapata vitambulisho, tuliahidi hapa Mheshimiwa kwamba mwaka huu tunashukuru Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweza kutupatia 17,000,000,000 ambazo zilikuwa zinadaiwa na mkandarsi na tumeshamlipa, kinachoendelea ni kuanza kutekeleza kadi ghafi ambazo zilisimama uzalishwaji wake kutokana na masuala ya UVIKO. Lakini tunayo matarajio kwamba ndani ya miezi sita ijayo tunaweza kuanza kupokea na wananchi wake watapokea vitambulisho kama ambavyo vitagaiwa kwa wananchi wengine, nashukuru.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN. MWINYI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga ofisi ya NIDA katika wilaya ya Mkoani?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Je, Serikali haioni haja ya kupeleka Ofisi za NIDA kwenye kila Halmashauri badala ya kwenye kila Wilaya ili kusiogeza huduma za wananchi hususani katika Halmashauri ya Msalala?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba inaweza ikaonekana umuhimu wa kuzipeleka ofisi hizi kwenye ngazi ya Halmashauri, lakini shughuli za NIDA ziko sehemu ya Serikali Kuu, na kama sehemu ya Serikali Kuu iko chini ya Mkuu wa Wilaya, ndiyo maana tumeanzia pale. Pale ambapo kutakuwa na haja, kwa mfano Wilaya yenye majimbo zaidi ya moja, tutaona uwezekano wa kuimarisha huduma hizo kwenye majimbo ya mbali na makao makuu ya wilaya, ili wananchi hawa waweze kupata hizo huduma stahiki.