Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini fedha itatengwa kufanya usanifu na upembuzi yakinifu wa Mradi wa kutoa maji Ziwa Nyasa kupeleka Tarafa ya Masasi – Ludewa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, hasa kwenda kwenye chanzo cha uhakika. Pamoja na majibu hayo mazuri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mlangali na Lugarawa ni kata ambazo zina ongezeko na kasi ya idadi ya watu tofauti na uwepo wa huduma za maji. Nini mpango wa Serikali kutenga fedha hizo kwenye bajeti ijayo ili kata hizo mbili ziweze kupata maji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kitongoji cha Lutala la Kisaula, vina idadi kubwa ya wananchi na hadhi ya vijiji, lakini kwa muda mrefu vimekuwa na changamoto ya maji. Mheshimiwa Naibu Waziri, alishaelekeza wataalam wa-extend Mradi wa Iwela kuhudumia maeneo hayo...

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa.

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, je, ni lini maelekezo hayo ya Serikali yatatekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mlangali na Lugarawa Mheshimiwa Mbunge, tulikwenda na tumeshudia kwa pamoja, lakini tayari kama Wizara tunaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili tuweze kutumia vyanzo vile vya uhakika; ile mito yetu miwili, Mto Salali na Mto Mbiliwili. Tutahakikisha tunatumia mito hii pale ambapo usanifu utakapokamilika na kuonekana na maji ya kutosha, ndiyo mto ambao tutautumia. Hili Mheshimiwa Mbunge amefuatilia kwa muda mrefu na tulikwenda pamoja.

Mheshimiwa Spika, vile vile, masuala ya Kitongoji cha Kisaula na Lutala, wakati Mheshimiwa Waziri anahitimisha hapa hoja za bajeti yetu ya mwaka 2023/2024, tayari imeonesha tumetenga Shilingi milioni 20.7 kwa ajili ya kufanya upimaji, usanifu na kupanua mtandao wa maji kutoka Mradi wa Maji Iwela. Kwa hiyo, hili tayari tumeshalifanyia kazi. (Makofi)