Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: - Je, tangu kuanzishwa kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ni kiasi gani cha fedha kimewekezwa na nini faida na hasara za uwekezaji huo?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu lilikuwa linasema faida na hasara ya uwekezaji. Umeniambia kiasi cha uwekezaji kilichowekezwa lakini hujaniambia faida na hasara ya kifedha. Kwa sababu inasemekana kwamba uwekezaji unafanywa kwenye maeneo yasiyokuwa na tija. Kwa hiyo, naomba nijibiwe swali la faida na hasara ya kifedha. Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, moja ya miradi mipya ni mradi wa Mkulazi kwa ajili ya uzalishaji wa Sukari. Pia, kwa mujibu wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambae wewe umemrejea anasema, Mipango duni ya utekelezaji wa mradi huu mpya ambao fedha za mifuko zinatumika, umesababisha gharama ya uwekezaji kuongezeka kwa bilioni 79, moja, hasara ya miaka ya miwili mfululizo ya bilioni 20.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu, unadhani mna matatizo gani linapokuja suala la uwekezaji kwa kutumia fedha za mifuko?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, kuhusu swali lake la kwanza kuhusiana na faida na hasara lilikuwa linauliza tangu kuanzishwa kwa mifuko ni kiasi gani cha fedha kimewekezwa na lakini eneo la pili, lilikuwa linauliza katika kila mfuko nini faida na hasara za uwekezaji? Kwa hiyo, ilikuwa ni faida na hasara sio fedha. Hata hivyo, tumeeleza kwenye eneo la fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la fedha miradi ambayo imewekezwa nimeeleza kwenye swali la msingi kwamba ni zaidi ya shilingi trilioni 14. 4 ambayo imewekezwa katika mifuko miwili kwa maana ya PSSSF zaidi ya shilingi trilioni 7.4 lakini pia kwenye NSSF ni trilioni 6.3. Sasa kwa fedha ambazo ni hasara haiwezi kuwa counted ni hasara kwa sababu uwekezaji ule ni endelevu na umeendelea kuwa wanaendelea kulipa kila wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika principle za uchumi ni sawa na kupwa na kujaa kwa bahari. Wakati wa uwekezaji tunaofuata ni mwongozo unaotolewa na Benki kuu ya Tanzania ambayo inaeleza maeneo ya uwekezaji. Pili, inaeleza namna gani ambayo watakwenda kuwekeza pamoja na ukomo wa kiwango cha kuwekeza fedha hizo. Kwa hiyo, hiyo unaweza ukaja ukaiona katika miradi na mingine imekuwa inawekezwa ikiwa ni inatoa huduma kwa wananchi. Kwa mfano; daraja la kigamboni na majengo mengine ambayo ni ya mifuko hii yameendelea kupata fedha kulingana na hali ilivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye swali lake la pili ambalo ameuliza kuhusu uwekezaji kwenye mfuko wa Mkulazi na ameeleza kuhusiana na Taarifa za CAG. Msingi ni ule ule kwamba Mkulazi kwa sasa hatujaanza uzalishaji lakini katika maeneo yale yaliyoainishwa utakumbuka vizuri wakati wa Uwekezaji BOT inatoa kanuni na miongozo na inaeleza maeneo ya uwekezaji na tatu inaeleza hadi ukomo wa uwekezaji.