Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua tatizo la ukosefu wa maji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba kuuliza;
Je, Serikali ina mikakati gani mahususi ya kutatua tatizo la maji lililoko sasa hivi katika Wilaya ya Longido?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Swai, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi ambayo iko Longido yote iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji, na lengo ni kuhakikisha tunakamilisha miradi hii kwa wakati.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua tatizo la ukosefu wa maji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, huu ni mwaka wa nane Serikali iliahidi kupeleka maji katika Kata za Makanya, Mlola, Kwai, Kwekanga hadi Kilole.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake hii ya kupeleka maji katika maeneo hayo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye kata hizi zote alizozitaja Mheshimiwa Mbunge tuna miradi ambayo tunaielekeza katika mwaka wa fedha ujao. Lakini vilevile maeneo yote ambako miradi tulishaanza kuitekeleza tutakwenda kuikamilisha. Mheshimiwa Mbunge hili tumeshajadiliana muda mrefu na ameshafika ofisini mara nyingi. Naomba nimpe ahadi kwamba baada ya hapa kama tulivyokubaliana tutakwenda na tutahakikisha miradi ile tunaifanya vizuri.