Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, lini Mahakama ya Wilaya ya Nyasa itaanza kujengwa?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nashukuru kwa kuianzisha mahakama hiyo. Kwa kuwa Mahakama ya Wilaya ya Nyasa inatumia majengo ya watu binafsi ambao pia wanaweza kuvunja sheria na kutakiwa kushtakiwa katika Mahakama hii;

Je, Serikali haioni kuwa kwa kufanya hivyo inaweza kuwafanya wadau wengine kutokuwa na Imani na Mahakama katika kutoa haki?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Mahakama za mwanzo za Tingi na Litui ni chakavu sana.

Je, ni nini mpango wa Serikali katika kuboresha Mahakama hizi?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru naomba sasa nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella kama alivyouliza. Swali lake la kwanza, anasema jengo hili la Mahakama ya Wilaya liko katika majengo ya watu binafsi, na anapata wasiwasi kama Mahakama inaweza ikatenda haki pale ambapo mtu huyu ambako tumepanga kwake ana jambo na Mahakama.

Mheshimiwa Spika, nikuhakikishie kwamba muhimili wetu wa Mahakama umeona jambo hili, ndiyo maana tumetenga fedha ili kuhakikisha mwaka huu wa fedha tunajenga Mahakama takribani 24 za Wilaya. Kwa hiyo sisi tutaipa kipaumbele Mahakama hii, na kwa kuwa kazi imeshaanza Mheshimiwa Manyanya awe na imani tu kwamba jengo hili litakamilika ili pasiwepo na wasiwasi wowote, japo Mahakama siku zote inatenda haki.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili amependa kufahamu, kwamba hizi Mahakama za kata ambazo zimetajwa zitajengwa lini na kwamba zimechakaa sana. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Mahakama yetu ya Tanzania imeliona jambo hili, na ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha tumetenga ujenzi wa Mahakama 60 kote nchini. Mahakama inafanya tathmini kujua kata zipi zipo mbali, na mpango wa Mahakama ni kujenga Mahakama katika maeneo ya tarafa ili kuhakikisha kwamba tunatoa huduma. Na taratibu tutaendelea kufikia kama bajeti utaruhusu kwenye hizo kata ambazo uhitaji umeonekana. Ahsante.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, lini Mahakama ya Wilaya ya Nyasa itaanza kujengwa?

Supplementary Question 2

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali inaendelea kujenga majengo mapya katika maeneo mbalimbali.

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama katika Wilaya ya Mbinga na Songea?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka huu wa fedha nimesema kwamba tuna Mahakama 24 tumeziitenga kuzijenga na Wilaya yake ni miongozni mwa wilaya hizo mabazo tutajengea Mahakama. Ahsante.