Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Soko la Samaki Kilwa Kivinje?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuambatana na Mheshimiwa Ally Kassinge kutembelea eneo la Kilwa Kivinje ili kujiridhisha na mahitaji ya soko hilo na kuharakisha ujenzi wake?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Ziwa Bassotu ukanda upande wa Kata ya Mulbadaw miundombinu ya msingi imeishajengwa ya mwalo. Je, yupo tayari kutoa tamko ili watendaji wake ndani ya Wilaya Hanang’ wafungue Mwalo huo mara moja? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge mara baada ya Bunge hili kuhairishwa na ratiba yetu tutapanga kuanzia mwezi ya saba kwa hiyo hilo limekubalika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu tamko la ziwa niseme tu kwamba, nimelipokea jambo hilo na ninakwenda kulifanyia kazi na baada ya hapo tutatoa tamko rasmi, ahsante.