Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikalii itajenga barabara ya mchepuko ya Mlima Nyoka (Uyole) hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe ili kuondoa msongamano na ajali?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri haya ya Serikali. Lakini naomba nikupongeze wewe mwenyewe kwa jitihada hizi na sasa kweli maendeleo ya Mbeya na Mbeya imetulia. Swali langu la kwanza je, ni lini sasa wananchi waliyopisha hii barabara wataanza kulipwa fidia? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Kuna barabara ya kiungo muhimu cha Mkoa wa Songwe pamoja na nchi jirani ya Malawi. Barabara ya Mbalizi – Shigamba ni lini Barabara ya Mbalizi – Shigamba itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii itaanza kujengwa kwa EPC+F ili kupunguza msongamano katika Jiji la Mbeya. Hii inaenda sambamba na ujenzi wa barabara ya njia nne kilomita 29 Uyole hadi Ifisi ambayo tayari Mkandarasi yuko site. Sasa kuhusu fidia ni kwamba fidia itaanza kulipwa mara tutakapokuwa tumehakiki wale wananchi wote ambao walishaainishwa kwamba watalipwa kwa mpango wa sasa kwamba kabla atujaanza kujenga hiyo barabara tutahakikisha kwamba fidia inalipwa kwenye barabara hiyo ambayo wananchi watapisha ujenzi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala lake la pili Barabara ya Mbalizi – Shigamba ambayo inakwenda mpaka Itumba – Isongole mpakani na Malawi. Nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba sasa hivi tunakamilisha na anafahamu Mheshimiwa Mbunge tunakamilisha kufanya usanifu wa kina na tunategemea mwaka huu tutakamilisha na baada ya hapo sasa utaratibu ni kuijenga barabara hiyo yote kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikalii itajenga barabara ya mchepuko ya Mlima Nyoka (Uyole) hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe ili kuondoa msongamano na ajali?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa ahsante, zabuni ya ujenzi wa kilometa nane za awali kwa Barabara ya Dareda – Dongobesh imetangazwa zaidi ya mara mbili. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo itaanza kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni kweli tulishatangaza lakini tumeitangaza tena nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba barabara hii kilomita zote zilizotangazwa kilomita 8 tutaijenga katika kipindi hiki shida ilikuwa tu baada ya kutangaza hatukumpata mkandarasi sahihi. Kwa hiyo, mpango upo na tayari tumeishaitangaza upya na tuko kwenye mazungumzo na mkandarasi ambaye ataijenga. Kwa hiyo, tutakapokuwa tumeikamilisha hayo mazungumzo barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.