Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa nyumba za Watumishi nchini hasa katika Halmashauri mpya?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa shirika hili limekuwa linajenga nyumba katika halmashauri mpya zilizoko mjini. Je, ni lini sasa shirika hili litaanza kujenga nyumba za watumishi katika halmashauri zilizoko vijijini hasa katika Halmashauri ya Ushetu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa Serikali inakuwa inapeleka fedha nyingi za ujenzi wa madarasa, zahanati na hospitalini lakini watumishi hawana nyumba kabisa. Ni lini mkakati wa Serikali kuwajengea nyumba watumishi hawa hasa walioko vijijini?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing) limeendelea kujenga nyumba katika maeneo mbalimbali. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Ushetu kwa kuwasemea watumishi wetu walioko katika maeneo na hasa Ushetu huko, kitu kikubwa kabisa ambacho tunaweza tukaahidi ni kwamba tunaendelea katika hatua mbalimbali za ujenzi na katika muda wowote ule tutafika huko Ushetu.

Mheshimiwa Spika, ombi letu sisi kama Wizara nikuomba halmashauri zote kutenga maeneo ambayo wangependekeza kujenga nyumba hizi zinazosimamiwa na mashirika kama hiyo National Housing na Watumishi Housing.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili; fedha nyingi zimepelekwa katika hizi mamlaka zetu za halmashauri kupitia TAMISEMI, na nimeona kwa sehemu kubwa sana fedha zinazopelekwa zinakuwa na kiambata cha nyumba za watumishi.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi kwa kupitia mashirika yetu haya taasisi zinazojenga nyumba zetu za watumishi. Sisi kama Wizara ya Ardhi tutaendelea kusimamia ujenzi wa nyumba hizo lakini niwahimize tu vilevile kwenye halmashauri wanapopata fedha zinazotoka Serikali kuu basi katika ile matumizi wajibane waweze kuweka na nyumba kiasi za watumishi wao katika maeneo wanapo pokea fedha zao. (Makofi)

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa nyumba za Watumishi nchini hasa katika Halmashauri mpya?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Kakonko na halmashauri yake ni mpya na hivi watumishi hawana nyumba za kuishi je lini Serikali sasa itajenga nyumba kwa ajili ya watumishi waliyoko katika Wilaya ya Kakonko? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kakonko na maeneo yote ambayo ni halmashauri mpya niwaombe kama nilivyosema kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Ushetu kwamba tutenge maeneo. Kwa sababu wakati mwingine mkienda kwenye maeneo hayo unakuta hakuna hata maeneo yaliyotengwa na halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za taasisi kama National Housing na Watumishi Housing.

Mheshimiwa Spika, hata hizi nyumba zilizopo bahati mbaya sana inatokea watumishi wengi hawaendi kukaa kwenye hizi nyumba na badala yake mashirika haya yamekuwa sasa yakipangishwa watu wa kawaida na hiyo ni mifano ipo hata hapa Dodoma tunazo nyumba nyingi pale Iyumbu lakini watumishi hawaendi pale kwa ajili ya kuzitumia. Ahsante.