Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwanza naipongeza na kuishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwa ajili ya bonde hili moja. Tunaiomba Serikali itupatie fedha kwa mwaka unaofuata kwa ajili ya Bonde la Kwamngumi pamoja na Bonde la Kwamsisi kwenye Halmashauri yetu ya Korogwe Mjini.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Dkt. Alfred James Kimea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumepokea maombi yake na kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, tayari Kwamngumi tumeshaingiza katika Mpango wa mwaka 2023/2024 kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Hivyo nimwondoe hofu, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba inawekeza katika miundombinu ya umwagiliaji. Tutapitia tena na maeneo mengine ambayo ameyataja hasa katika eneo la Kwamsisi.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa. Je, ni lini mradi wa umwagiliaji wa Mwamapuli uliopo Halmashauri ya Mpimbwe utaanza kujengwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ukisoma katika kitabu chetu cha kwenye bajeti kiambatisho Na. 6, kimeelezea skimu ambazo tunakwenda kuzifanyia kazi kwa maana ya ujenzi kwa mwaka 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, skimu ya Mwamapuli yenye hekta 12,000 Wilaya ya Mpimbwe ni sehemu ya utekelezaji wa ujenzi wa katika mwaka wa fedha unaokuja. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge skimu hiyo inakwenda kutekelezwa.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba tu kujua Serikali itaenda lini kuangalia skimu ya umwagiliaji ya Kisango na skimu ya umwagiliaji ya Mariwanda ili kuifanyia kazi. Lini mtaenda kuangalia skimu hizo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha skimu zote zinafanyakazi ili tuongeze eneo la kilimo cha umwagiliaji. Nataka nimuhaidi Mheshimiwa Mbunge, kwamba nitawaelekeza watalamu wangu kwenda kupitia maeneo ambayo ameyataja ili tuweze kupata picha halisi na tuingize kwenye mpango. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itaendeleza Ujenzi wa skimu ya Kijiji cha Mwagrila baada ya kutumia shilingi bilioni 1.2 na haikuwa kwenye mpango wa Serikali? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tulituma watalamu kupitia skimu zote nchi nzima, zile ambazo zilikwama na zile ambazo zinahitaji marekebisho tumeishatengeneza picha nzuri ya kuzijua zote pamoja na hiyo ambayo ameitaja nataka nimtoe hofu ya kwamba ipo ndani ya mipango ya Serikali tutaitekeleza.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza je, ni lini mradi wa Mgambalenga katika kata ya Ruaha Mbuyuni utakamilika, kwa sababu toka mwaka 2014 umeanza kujengwa lakini haupatiwi pesa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika skimu 42 ambazo zilifanyiwa upembuzi yanikifu na usanifu wa kina katika mwaka wa fedha 2022/2023 ni pamoja na skimu ya Mgambalenga. Hivyo katika Mwaka 2023/2024 skimu hii itaendelea kufanyiwa ukarabati wa miundombinu na kazi itafanyika kwa uharaka zaidi ili wakulima waweze kupata fursa ya kufanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)