Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha ukusanyaji mapato kwa biashara zinazofanyika mtandaoni?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, ila nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tayari Serikali ina kitengo maalum na tayari inafanya utambuzi na ukusanyaji wa kodi hizi: Je, tangu jitihada hizi zifanyike, mapato yanayotokana na biashara hizi yameongezeka kwa kiasi gani?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Pamoja na mikakati mizuri ambayo Serikali inafanya, bado biashara nyingi za kimtandao hazijafanyiwa utambuzi na hazifanyiwi ukusanyaji ikiwemo biashara ya D & D; Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha mikakati hii ili biashara hizi ziweze kufanyiwa utambuzi wa ukusanyaji mapema ili kuongeza mapato? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Judith, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la kwanza ni kiasi gani, naomba hili nijibu kwa njia ya maandishi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, Serikali imeendelea kulipa VAT na kwa taratibu zote na imechukua suala hilo na inaendelea kulifanyia kazi.