Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha huduma za dialysis kwa Wagonjwa wenye kipato cha chini?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Je, Serikali imejipangaje katika kupunguza gharama za huduma hii ya dialyisis, kwani kwa sasa ni shilingi 200,000 hadi shilingi 350,000 kwa mgonjwa anapoenda kuhudumiwa kwa mara moja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kutokana na majibu ya Serikali, napenda kufahamu, ni utaratibu upi mgonjwa ambaye ana kipato kidogo afuate ili aweze kupata msamaha wa huduma hii ya usafishaji wa figo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, lakini niseme, moja ni kwamba kwenye bajeti hii ambayo tunaiwasilisha sasa, mpaka jana tulikuwa tunakaa kuangalia maeneo mawili. Waziri wetu ameangalia kwenye eneo la mama na mtoto na eneo hili, na tumegundua kuna uwezekano badala ya tiba hii kuwa shilingi 350,000, inawezekana kabisa mtu akatibiwa kwa shilingi 90,000 hadi shilingi 150,000. Kwa hiyo, tuna mpango huo wa kushusha gharama hizi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kwamba, mtu afuate utaratibu gani? Moja, akishakuwa na barua ya Mtendaji wake wa Kata, hiyo inatosha kumfanya aweze kupewa exemption, ndivyo utaratibu unavyosema.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha huduma za dialysis kwa Wagonjwa wenye kipato cha chini?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Je, ni lini Serikali itaanzisha huduma hii ya usafishaji figo katika Mkoa wetu wa Katavi?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwenye hospitali yao mpya ya Mkoa wa Katavi tayari vifaa vimenunuliwa, sasa hivi wako kwenye finishing ya aneo ambalo linatakiwa hivyo vifaa visimikwe halafu huduma hii itaanza mara moja kwenye mkoa wenu wa Katavi. Hata CT- Scan ambayo Rais wetu ameinunua imeshafika.