Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na ongezeko la Wagonjwa wa Kansa ya Kizazi?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Taasisi ya Kansa ya Ocean Road Dar es Salaam imekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa siku hadi siku na idadi kubwa ya wagonjwa ambayo inaongezeka hapo ni akina mama wenye matatizo ya kansa ya kizazi: Je, Serikali haioni haja sasa kuwasaidia akina mama hawa kufungua vituo vya kansa katika hospitali za kanda na mikoa ili kupunguza gharama za usafiri kwa akina mama hao na mahitaji muhimu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali imeonesha kwamba kuna huduma za awali za uchunguzi wa kansa katika hospitali mbalimbali: Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuziunganisha huduma za uchunguzi wa awali za kansa katika kliniki zetu za mama na mtoto ili mama apate huduma hiyo kabla na baada ya uzazi? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya ya kufuatilia eneo hili la afya ya akina mama. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake la kwanza kwamba Serikali yetu imejipanga, ndiyo maana mmetusikia hapa tukisema Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kwa mwaka huu tu shilingi bilioni 290.9 kwa ajili ya kuleta vifaa tiba. Kwa hiyo, kwenye hospitali zetu za kanda na mikoa, vifaa vile vitasaidia kuchunguza, lakini kwenye kanda wanatibiwa kabisa. Kwa hiyo, hiyo huduma imepelekwa, kanda watatoa, mikoa watatoa. Tuliona juzi madaktari waliokuwepo hapa, kazi yao mojawapo ni kwenda kuhakikisha wanatambua mambo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwenye maana ya kufika kule wilayani, labda nikwambie tu, tunalichukua, tunaliongezea nguvu lakini wenzetu waliokuja hapa pia mojawapo ya kazi yao ni kukutana na akina mama mpaka kwenye vituo vyetu na zahanati, wakiendelea kuhakikisha kwamba mojawapo ya jambo la kuzingatia ni kuangalia hiyo saratani ya kizazi, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na ongezeko la Wagonjwa wa Kansa ya Kizazi?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na Waganga wa Jadi na wa Asili ambao wamekuwa wakibaini kwamba wao wanatibu kansa mbalimbali: Nini kauli ya Serikali kuhusiana na waganga hao ambao wamekuwa wakiwapa wagonjwa taarifa ambazo siyo sahihi? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kauli yetu ni moja tu kwamba, yeyote atakayeibuka akiwa na jambo hilo, moja, tunatuma watu wetu wa Mkemia Mkuu, lakini taasisi ya tiba asili kuhakikisha na kukiangalia kile anachokisema kama ni kweli. Tunapogundua siyo tiba, tunamzuia kufanya hivyo na tunamtia moyo wa kuendelea kufanya utafiti na kufikiria namna ya kutatua kwa pamoja kwa kushirikiana na sisi. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na ongezeko la Wagonjwa wa Kansa ya Kizazi?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwa kuwa swali la msingi linauliza kuhusu ongezeko la kansa, mimi nilitaka kufahamu: Je, Serikali imefikia wapi katika kufanya tafiti kwenye mikoa ya kanda ya ziwa na suala zima la ongezeko kubwa la magonjwa ya kansa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, hatua tuliyoifikia tayari tumeshachukua sample kwa watu mbalimbali zaidi ya 700, na sasa ziko kwenye maabara kwa ajili ya kuchambua kwenye level ya genetics ili kuona hasa ni nini tatizo linalosababisha hali hiyo kule kanda ya ziwa.