Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, kwa nini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Nansio haifanyi kazi?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa vile Mamlaka ya Mji mdogo wa Mbalizi kwa muda mrefu sasa imeshakua, na ina uchumi mkubwa, ni lini Serikali itaipandisha hadhi kuwa Halmashauri ya Mji wa Mbalizi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kuhusu kupandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo Mbalizi kuwa Halmashauri ya Mji, kwa sasa Serikali inamalizia kwanza majengo ya kiutawala na huduma za kijamii katika mamlaka ambazo zipo tayari. Baada ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu katika mamlaka hizi, tutaanza sasa kuangalia ni wapi panahitaji napo kupandishwa hadhi na kuwa mamlaka ya mji kama vile kule Mbalizi?

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, kwa nini Mamlaka ya Mji Mdogo wa Nansio haifanyi kazi?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mamlaka ya Mji Mdogo Namanyere, tumeshafanyiwa tathmini na tumekidhi vigezo: Ni lini sasa tutapandishwa hadhi kuwa mamlaka ya Mji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Mji Namanyere kupandishwa hadhi itakuwa ni baada ya Serikali kumalizia ujenzi wa miundombinu katika Halmashauri, Mamlaka za Miji na Majiji ambayo yamehama katika maeneo yao ya kiutawala, na sasa Serikali inapeleka fedha nyingi kumalizia maeneo hayo.