Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari Mkalapa itatambuliwa kuwa shule ya vipaji vya michezo ya mpira wa wavu?

Supplementary Question 1

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ninapenda kujua sasa ni lini Serikali itaanza kuimarisha miundombinu ya shule hizo 56 lakini niombe na miundombinu ya Shule ya Mkalapa pia iboreshwe?

Swali la pili, ninapenda pia nijue Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba shule zote zinapata walimu wa michezo ili kusudi vijana wetu waweze kushiriki katika michezo kikamilifu? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itaboresha miundombinu ya shule hizi 56 ikiwemo kama nilivyosema tathmini inafanyika katika Shule ya Sekondari Mkalapa ambayo imefanya vizuri sana katika michezo ya UMISETA lakini vile vile michezo ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo Serikali inafanya tathmini na itaijumlisha na yenyewe Shule ya Mkalapa na tutatafuta fedha na kwenda kujenga miundombinu kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la walimu wa michezo. Katika ajira ambazo Serikali imetangaza hizi 21,000 ambapo 13,390 hizi ni ajira za walimu. Tutaangalia ni namna gani nayo tuna-accommodate walimu wa michezo, walimu wa kilimo, walimu wa ufundi ili kuweza kuboresha elimu yetu hapa nchini.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni lini Shule ya Sekondari Mkalapa itatambuliwa kuwa shule ya vipaji vya michezo ya mpira wa wavu?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari Ngoreme Wilayani Serengeti kumekuwepo na jitihada nyingi za wananchi na wadau mbalimbali za kujenga miundombinu kwa lengo la kuifanya kuwa shule ya Kidato cha Tano na cha Sita. Yamekuwepo maombi yangu mbalimbali mara kadhaa kwa TAMISEMI.

Je, ni lini sasa TAMISEMI mtaipandisha hadhi shule hii kuwa ya Kidato cha Tano na cha Sita?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Amsabi Mrimi kwa jitihada zake za kuhakikisha shule hii ya Ngoreme inapandishwa hadhi. Kwa sasa walikuwa wanamalizia ujenzi wa mabweni ili kuweza kuhakikisha kwamba shule hii inakidhi vigezo vya kuwa A level na baada ya hapo Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Elimu zitafanya jitihada za kuhakikisha shule hii inasajiliwa kuwa na mkondo wa Kidato cha Tano na Sita.