Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za Askari Polisi katika Kituo cha Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Hadi sasa katika Wilaya ya Micheweni hakuna nyumba za askari ambazo ujenzi unaendelea. Pamoja na hili sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kituo cha polisi Wilaya ya Micheweni ndiyo Makao Makuu ya Polisi Wilaya ya Micheweni. Je, Serikali ina mkakati gani wakujenga nyumba za polisi katika Wilaya ya Micheweni? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika kituo cha polisi cha Wilaya ya Micheweni kuna hanga la Jeshi la Polisi ambalo lilijengwa kutokana na nguvu za wananchi miaka kumi iliyopita hadi sasa hanga hili kutokana na kwamba halikumaliziwa tayari limeanza kuharibika ikiwemo paa kuvuja na saruji kuharika. Je, Serikali haioni haja kuunga mkono jitihada hizi za wananchi kwa kumalizia jengo hili? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati nimeusema ni kuendelea kutenga fedha kujenga nyumba za askari na maofisa kutegemea upatikanaji wake hata hivyo alichosema kwamba ujenzi umesimama kule Micheweni Mheshimiwa Mbunge ni kweli ndiyo maana kwenye jibu la msingi nimesema zinahitajika milioni 60 ili kumalizia jengo hilo na fedha hizi zinatengwa kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024 kutoka Mfuko wa Tuzo na Tozo. Kwa hiyo, Mheshimiwa eneo hilo litakamilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uendelezaji wa ujenzi wa nyumba, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi tutaendelea kujenga nyumba za askari kadri tunavyopata pesa kwenye bajeti yetu au pale tunaposhirikiana na wadau.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.