Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Kata za Mkalamo, Magamba Kwalukonge na Mkomazi Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Kata ya Mpare yenye vijiji vinne na chanzo kizuri cha maji hakuna kijiji hata kimoja chenye maji. Ni lini Serikali itatatua changamoto ya maji kwenye Kata ya Mpare?

Swali la pili, mradi wa maji wa Goha, Mkumbara mkandarasi wake amekuwa akisuasua na kwa muda mrefu kazi zimesimama. Pamoja na maelekezo uliyotoa Mheshimiwa Waziri hakuna kinachoendela. Ni nini kauli Serikali juu ya mradi huu? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayofanya, lakini kubwa ambalo nataka nimhakikishie hasa katika hii Kata ya Mpare katika bajeti yetu hii ambayo tunakwenda 2023/2024 tumezingatia ombi lake katika kuhakikisha wananchi wanapata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya mradi huu ambao Mkandarasi ana suasua nilishafanya ziara Korogwe, moja ya maelekezo ambayo tumeyatoa mkandarasi yule aondolewe mara moja pale site na kazi ile tutaifanya kupitia wataalam wetu na kuweza kukamilisha kazi kwa wakati. (Makofi)

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Kata za Mkalamo, Magamba Kwalukonge na Mkomazi Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 2

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kata ya Kikolo na Kilimani pia Vijiji vya Mtama, Tukuzi, Masmeli na Mateka. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kujenga miradi katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, Jumatano kwa maana ya Tarehe 10 nawasilisha Bajeti yetu ya Wizara ya Maji kwa hiyo mambo yatakuwa ni fire, mambo ni moto. Ahsante sana. (Makofi)