Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti katika maeneo yanayoonekana kuwa na madini ili wananchi wanufaike?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuulizwa maswali mawili ya nyongeza.

Swali langu la kwanza, je, ni kiasi gani GST imewezeshwa kufanya kazi?

Swali langu la pili, je, Serikali ina mpango gani mahsusi kuhakikisha Watanzania wananufaika na madini haya yanayopatikana nchini Tanzania? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Kainja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la kwanza GST katika bajeti hii ambayo ilipitishwa na Wizara ya Madini imetengewa kiasi cha fedha shilingi bilioni mbili na milioni mia nne kwa ajili ya shughuli zake mbalimbali ikiwemo kipande kidogo kwa ajili ya utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, shughuli hizi za utafiti zinahitaji fedha nyingi sana kwa hiyo shilingi bilioni 2.4 peke yake haitoshi, wenzetu wa GST tayari wameshaanza kufanya proposal za kupata fedha kutoka maeneo mengine ili kuweza ku-complement kwenye zile fedha ndogo ambazo wanazo kwa ajili ya kukamilisha hii kazi ambayo wamepatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili ni mkakati wa Serikali ambao unafahamika wazi kwamba madini yanayochimbwa Tanzania yanawanufaisha Watanzania wote, uniruhusu nitoe mfano mmoja kwa juzi Barrick imetoa CSR kiasi cha shilingi bilioni 30 ambayo kwa kuanzia imetoa Shilingi Bilioni 10, hata sisi ambao hatuko katika yale maeneo ya mgodi tumepata fedha hiyo. Kwa hiyo, Watanzania wote Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha kwamba kila mmoja anayetakiwa kunufaika nayo ananufaika kwenye eneo lake.