Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa barabara hiyo inategemewa kiuchumi kutoa mazao sokoni, kupitisha watalii kwenda Mahale, na kwa kuwa mara nyingi Serikali imekuwa ikijibu upembuzi yakinifu, usanifu kwa muda mrefu, zaidi ya miaka mitano.

Je, Waziri anaweza akanihakikishia kabisa ni lini sasa barabara hiyo itaanza? (Makofi)

Swali langu la pili, kwa kuwa Kivuko cha Ilagala huanza kazi saa 12 na kuishia saa 12 na kinategemewa na Kata ya Sunuka, Sigunga, Helembe na Kalya, saa 12 mawasiliano yanakuwa yamekatika.

Je, kwa nini Serikali isiongeze muda kivuko kikafanya kazi mpaka Saa Sita usiku? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi tunavyoongea consultant kwa maana ya mhandishi mshauri yuko kazini kwa ajili ya kusanifu hilo Daraja la Malagarasi. Kwa hiyo tayari Serikali imeshaanza kufanya kazi, siyo tena hadithi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa ajili ya kuongeza masaa naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaangalia uwezekano wa kuongeza masaa kadri itakavyowezekana. Pia Serikali inaona suluhu ni kujenga daraja kwenye hicho kivuko na ndiyo kazi ambayo inafanyiwa usanifu ili badala ya kuwa na kivuko ambacho kinafanya kazi kwa masaa tujenge daraja la kudumu ambalo tutanfanya kazi muda wote.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri ni lini barabara ya Bujela – Masukulu hadi Matwebe itawekwa katika kiwango cha lami katika Wilaya ya Rungwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali ni kujenga barabara zote za lami, tutashirikiana na wenzetu wa TARURA kuona kwamba hii barabara nayo inaingizwa kwenye usanifu na hatimaye iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?

Supplementary Question 3

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri ni lini, kwa sababu kivuko hicho ambacho amekizungumza eneo hilo lina giza sana. Je, ni lini ataweka taa kwenye eneo hilo la kivuko?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge naomba nichukue wazo lako na tuangalie uwezekano wa kuweka taa kwenye hilo eneo la kivuko ambalo linaunganisha hizo pande mbili kwa ajili ya kusaidia kufanya kazi muda wa usiku.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?

Supplementary Question 4

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Nangwa – Gisambala – Kondoa ikiwepo Daraja la Munguri kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja tuna mpango nayo kwa ajili ya kukamilisha na ku-review usanifu na baada ya hapo gharama zitajulikana ili tuweze kuipanga sasa kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Simbo hadi Kalya?

Supplementary Question 5

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mlowo – Utambalila mpaka Kamsamba kila kitu kiko tayari, nyaraka za tender, usanifu wa kina. Sasa nilitaka nijue, ni lini Serikali itapeleka barabara hii kwa Mheshimiwa Rais kuombewa kibali cha kujengwa kwa njia ya lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mlowo – Utambalila hadi Kamsamba ni barabara ambayo tayari Serikali imeshajenga Daraja la Mto Momba na kumekuwa na maelekezo ya viongozi mbalimbali wa Kitaifa akiwepo Waziri Mkuu, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaiweka kwenye mapendekezo kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa bajeti ambayo tunaiendea mbele.