Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza nyumba za makazi kwa Askari Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; pamoja na maelezo yake nataka kujua ni lini ujenzi huo utaanza katika maeneo hayo ya Finya, Micheweni na Konde? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; naomba kujua Serikali imejipangaje kuhusu kuchimba visima katika maeneo hayo ambayo yatajenga hizo nyumba kwa sababu kama tunavyofahamu maeneo hayo yana uhaba wa maji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu lini ujenzi utaanza kwenye jibu langu la msingi nimeeleza kwamba ujenzi unaendelea kwenye maeneo tofauti. Kwa mfano, eneo la Finya kuna nyumba nne zinaendelea kujengwa na ziko kwenye hatua ya umaliziaji. Kuhusu uhaba wa maji tutashirikiana na mamlaka ya utoaji wa huduma za maji katika Wilaya ya Micheweni ili ishiriki kwa sababu si kazi ya polisi ku-supply maji, lakini pale tunapokuwa na uwezesho wa kifedha tunachimba visima vya maji, lakini kwa sasa bajeti tuliyotenga ni kwa ajili ya ujenzi wa vituo na makazi ya askari, nashukuru. (Makofi)

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza nyumba za makazi kwa Askari Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ushetu haina jengo lolote la Kituo cha Polisi na wanaendelea kuishi kwenye majengo ya kupanga, hakuna nyumba za maaskari, lakini sioni mkakati wowote wa Serikali juu ya suala hili toka mwaka jana nalilalamikia. Je, ni nini kauli ya Serikali?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunajua Ushetu ni wilaya mpya ilibebwa kutoka Kahama na ndio changamoto ya kuanzisha maeneo mapya ya makazi. Tunachokifanya katika Wizara ya Mambo ya Ndani, hususani Idara ya Jeshi la Polisi ni kuendelea na ujenzi wa maeneo haya hatua kwa hatua kadri tunavyopata bajeti. Nimuahidi Mheshimiwa Cherehani, nilishajibu hapa Ushetu ni eneo lenye kipaumbele kwa sababu ya shughuli za kiuchumi zilizoko huko. Wanahitaji kuwa na kituo cha polisi cha uhakika, kwa hiyo pale tutakapopata fedha kituo hiko kitajengwa, nashukuru.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza nyumba za makazi kwa Askari Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Katika Kituo chetu cha Polisi kilichopo katika Kata ya Somanga, Wilayani Kilwa chenye watumishi 19, hakina hata nyumba moja ya watumishi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwajengea nyumba watumishi hawa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendelea kujenga kadri ya upatikanaji wa fedha, maadam jengo la polisi lipo. Tutakachoendelea kufanya ni kuhakikisha kwamba eneo linapatikana na sisi tuingize kwenye bajeti kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Ndulane kama eneo limeshapatikana kwenye halmashauri husika, tuko tayari kushirikia nao kuhakikisha nyumba hizo zinajengwa, ahsante sana.