Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, Swali la kwanza; kwa kuwa wadau wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya na kumshirikisha RPC na OCD wamefikia hatua ya kutenga fedha na kuanza kujenga kituo hicho na Wizara mpaka sasa hawajatoa shilingi ya aina yoyote. Je, ni lini Serikali watapeleka fedha kwa kuwaunga mkono wananchi ambao wamejitolea kuhakikisha wanafanya kazi hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; halmashauri ya wilaya imetoa eneo na Serikali inatakiwa itoe shilingi milioni 20 kwa ajili ya kupata hati miliki. Je, ni lini sasa mchakato huo wa kupeleka hizo fedha utafanyika ili jitihada za kuejnga kituo hicho zianze kufanyika kwa wakati?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, lini fedha zitapelekwa? Hatua ya kwanza kama alivyomaliza swali lake la pili ni kulipa hii fedha ya fidia na upimaji ya milioni 20 na nimuahidi katika bajeti ijayo fedha zimetengwa zitapelekwa. Baada ya kulipa fidia na kupata hati Wizara itaji-commit kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ku-support nguvu za wananchi kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, ahsante sana.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Polisi katika Mji wa Njombe ni kichakavu sana na cha zamani. Je, ni lini ujenzi wa Kituo kipya cha Polisi utaanza?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia Jeshi la Polisi itaanza na kazi ya kufanya tathmini ya kiwango cha uchakavu wa majengo ya Kituo cha Polisi ngazi ya Wilaya cha Njombe. Iwapo itathibitika kwamba gharama za ukarabati zitakaribia kulingana na gharama za ujenzi wa kituo kipya, uamuzi utafanyika kwa ajili ya kujenga kituo kipya, lakini kama gharama zitakuwa manageable tutakikarabati kituo hicho ili kiweze kuwa cha kisasa zaidi, nashukuru.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tanganyika?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa fursa hii. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Polisi katika Kata ya King’ori kama ilivyoahidi mwaka jana? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyowahi kujibu kwa nyakati tofauti, ujenzi wa Vituo vya Polisi ngazi ya Kata ni jukumu la jamii kwa maana ya halmashauri na wananchi wake, lakini pale ambapo tunakuta juhudi hizo zimefanyika Wizara huunga mkono kupitia Jeshi lake la Polisi. Nimwombe Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, najua juhudi zake kwenye hili, waanze na sisi tutakuja kuwaunga mkono, ahsante sana.