Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhimiza vijana kushiriki shughuli za kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, vijana wanaoshughulika na kilimo katika Mkoa wa Kigoma wana changamoto ya mitaji.

Je, ni lini Serikali itawaongeza mitaji ili kuongeza tija katika shughuli za kilimo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, ni lini eneo la Mradi wa BBT lililotengwa na Serikali katika Mkoa wa Kigoma, mradi huu utaanza kutekelezwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza la kuhusu mitaji kwa ajili ya vijana wanaofanya shughuli za kilimo. Ni dhamira ya Wizara ya Kilimo na Serikali kwa ujumla kuhakikisha tunawawezesha vijana wote ambao wanashiriki katika kilimo ili waweze kufikia malengo na matarajio yao. Kupitia Mfuko wa Pembejeo hivi sasa tumeshaanza kutoa matangazo ya kuwakaribisha vijana wote ambao katika shughuli za kilimo kuja kuomba mikopo na mikopo yetu itakwenda katika riba ya chini kabisa ili vijana wengi waweze kunufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, katika eneo la Kasulu tunayo mashamba ya kilimo kwanza ambayo katika Kijiji cha Kwitanga na tunayo mashamba pia ya Makere ambayo katika vijiji vya Mgombe na Mvinza. Yote yana ekari elfu tano tano. Nataka nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba, baada ya vijana hao kumaliza mafunzo, tutaanza utekelezaji mara moja na vijana wa Kigoma watanufaika kupitia mradi huo.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhimiza vijana kushiriki shughuli za kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa fursa hii. Kwanza kabisa naomba niipongeze Serikali kwa jitihada zake zinazofanya kuhakikisha vijana wanashiriki kikamilifu kwenye shughuli za kilimo kupitia programu hii ya BBT. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha akinamama ambao ni wazalishaji wakubwa kushirikishwa kwenye mpango kama huu kama akinamama wa Mkoa wa Arusha? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiiangalia hii Programu ya BBT pia inahusisha na akinamama. Kwa hiyo akinamama wako ndani katika programu hii, natumai kwamba akinamama wa Mkoa wa Arusha pia watachangamkia fursa hii ya kushiriki kwenye kilimo. (Makofi)