Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti mafuriko ambayo husababisha uchafuzi wa mazingira na kuongeza umaskini katika Jimbo la Mwera?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishukuru Serikali kwa jibu lake lakini pia wamekuwa wanasiasa. Mimi ombi langu ni hili; kwa sababu hili siyo jambo la kupanga ni jambo la dharura, na tumeliuliza zaidi ya miaka mitatu humuhumu ndani majibu ndiyo hayahaya, ombi langu ituambie Serikali.

a) Je, ni lini imeamua au itaamua kulishughulikia jambo hili kwa dharura?

b) Je, ni lini sasa Serikali itashirikiana seriously na Serikali ya Zanzibar ili kuwaondolea maafa watu wetu wa Mwera?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Jimbo la Mwera kutoka Zanzibar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari ziko hatua mbalimbali ambazo zimeshachukuliwa kama hatua za dharura kwa sababu ya jambo hili la utokeaji wa haya maafa. Na hapa nataka nichukue fursa hii nimpe pole sana Mheshimiwa Zahor kwa haya matukio ambayo yanatokezea mara kwa mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitendo cha Serikali kuunda kamati zinashughulikia maafa ambazo zipo kwenye ngazi tofauti, zikiwemo ngazi za shehiya na ngazi za wilaya ni miongoni mwa hatua madhubuti ambayo imeshachukuliwa. Katika jibu la msingi tayari tumeshaeleza kwamba, kupitia bajeti hii ya mwaka ya fedha huu 2023/2024 tutahakikisha kwamba tunakwenda kushughulikia maeneo yote ambayo yanakabiliwa na maafa kama haya likiwemo Jimbo la Mwera na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine nataka tu nimwambie Mheshimiwa kwamba kuna baadhi ya mambo tayari tumeshayaelekeza. Serikali imetoa maelekezo kupitia Serikali ya Jamhuri na Serikali ya Zanzibar, kwamba kwanza watu waendelee kupewa elimu, ngazi za shehiya, halmashauri, wilaya, mikoa zitoe elimu kwa wananchi. Elimu ya kwanza, wananchi wasijenge kwenye mabonde, wasijenge kwenye maeneo ambayo maji yanatuama. La pili, wananchi wasitupe taka chafuzi, taka ngumu, taka zidishi kwenye maeneo ya mitaro, mwisho wa siku inakwama, halafu maji hayaendi yanasababisha mafuriko. La tatu, wajenge kwenye maeneo ambayo yameshapimwa. Lengo na madhumuni wajenge kwenye maeneo salama waepukane na maafa kama haya, nakushukuru.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti mafuriko ambayo husababisha uchafuzi wa mazingira na kuongeza umaskini katika Jimbo la Mwera?

Supplementary Question 2

MHE. FATUMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Eneo la Nkuhungu katika Jiji la Dodoma ni miongoni mwa maeneo ambayo yanaathiriwa sana na mafuriko mara kwa mara. Nini mkakati wa Serikali wa kutengeneza miundombinu mizuri ili kuwanusuru na mafuriko wananchi hawa wa eneo la Nkuhungu? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama Toufiq, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yapo maeneo ambayo hali iliyofikia sasa hakuna namna nyingine isipokuwa ni kutengenezewa miundombinu ambayo itakwenda kudhibiti hii hali na kuwaacha wananchi wakiwa salama. Nimwambie Mheshimiwa kwanza tutataka tufanye study, tufanye utaratibu maalum wa kufanya tafiti kujua nini kinatakiwa hapo, kama ni daraja au ni kivuko kingine chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, cha pili, tutafute fedha sasa, kwa sababu hivi vitu vinataka fedha. Nimwambie Mbunge awe na Subira, maeneo yote ambayo yanaelekea ama yameshaingiliwa na maji na yanasababisha mafuriko hasa kipindi cha mvua kubwa, Serikali kwa kupitia ofisi yetu itahakikisha kwamba tunayashughulikia, nakushukuru. (Makofi)

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti mafuriko ambayo husababisha uchafuzi wa mazingira na kuongeza umaskini katika Jimbo la Mwera?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Jimbo la Kawe katika maeneo ya Boko Basihaya, Boko Magengeni, Mto Nyakasangwe ni maeneo ambayo yamekuwa yakikumbwa na mafuriko kwa muda mrefu sana. Awamu ya Mheshimiwa Jakaya walishakwenda pale, Awamu ya Mheshimiwa Magufuli wameshakwenda pale na sasa hivi ni Awamu ya Sita. Je, Serikali ina kauli gani kuhusiana na kero hii kubwa inayosumbua wananchi? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: - (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba azma ya Serikali hii ya Mama Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba inatekeleza ahadi ambazo zilishaahidiwa, inatekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya kadri itakavyowezekana kuhakikisha kwamba tunakwenda kutengeneza miundombinu rafiki, itakayoondosha hiyo changamoto ya mafuriko na changamoto nyingine ambayo inakuwa ni kikwazo katika maendeleo ya kiuchumi hasa ya wananchi,, nakushukuru.