Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kukomesha vifo na upotevu wa mali kutokana na migogoro ya wakulima na wafugaji katika Wilaya ya Kilwa, Nachingwea na Liwale?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

a) Je, ni lini malambo ya kunyweshea maji mifugo hiyo yatajengwa maeneo ya Ngunichile, Kibutuka na Njilinji ili kuondoa migogoro hiyo?

b) Je, ni lini utengaji wa ardhi utafanyika katika maeneo ambayo kunatokea vifo na migogoro hiyo hususani Kibutuka na Njilinji, Ngunichile Natekwe na kwingineko?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la kwanza Mheshimiwa Ungele tutashirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweza kuona ni namna gani tutajenga kwa haraka sana haya malambo ya maji Mtekwe na Kimambi kuhakikisha kwamba mifugo iliyokuwepo kule inaweza kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, kuhusu upangaji wa ardhi, sheria zipo wazi, kuna Sheria Namba Tano ya Ardhi ya mwaka 1999 Toleo la 2002 juu ya matumizi bora ya ardhi ambapo inatoa mamlaka kwa vijiji kupanga matumizi bora ya ardhi ambapo wanatakiwa kutenga malisho, maeneo ya masoko, mashamba na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nichukue nafasi hii kwenye Bunge lako tukufu kuwaomba na kuwaasa viongozi katika halmashauri zetu nchini ikiwemo Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha wanasimamia sheria hii kwa kupanga matumizi bora ya ardhi ili kuepuka mogogoro ya ardhi na hasa ile ya wakulima na wafugaji.