Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali; lakini hata hivyo nina swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa barabara ni moja ya barabara ambazo wananchi wa Mbarali wanazitumia sana kusafirishia mazao na sasa barabara nyingi zimeharibiwa mno na mvua hali inayopelekea ugumu wa kufanya shughuli hizi.

Je, ni ipi kauli ya Serikali kwa wanambarali kuhusu adha hii?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge, barabara nyingi ambazo zimeharibika kutokana na msimu huu wa mvua zimewekewa kipaumbele cha matengenezo katika mwaka huu wa fedha tunaoenda kuuanza Julai, Mosi mwaka huu.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nataka nijue Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya mkato inayotoka Komaswa – Tarime Vijijini kuja mpaka Rorya kupitia Nyatorogo pamoja na Daraja lake la Nyatorogo kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024, kama ina mpango wowote wa ujenzi wa daraja pamoja na barabara hii? (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa unaweza ukataja vizuri hizo barabara zako kutoka wapi mpaka wapi?

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara inayotoka Komaswa – Tarime Vijijini kuja Rorya kwa kupitia Kata ya Nyatorogo ikiwa ni pamoja na daraja lake linalounganisha Tarime Vijijini pamoja na Rorya. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kwanza kuona kwamba barabara hii ni ya TARURA au ya TANROADS halafu kuona ni hatua gani ambazo tunaweza tukazichukua kuweza kufungua Barabara hii ya mkato ya Komaswa hadi Rorya. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti nishukuru kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kipindi hicho Ummy Mwalimu aliahidi shilingi bilioni 1.5 kuunganisha Wilaya ya Tanganyika na Wilaya ya Uvinza kupitia Kata ya Kalia na Kata ya Mwese.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi waweze kupata huduma? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa barabara hii ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutakaa na wenzetu wa TARURA kuona mpango wao juu ya kutenga fedha hii ya bilioni 1.5 ya kuunganisha barabara kati ya Tanganyika hadi Uvinza. (Makofi)

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE J. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniona. Barabara inayoanzia Chunya Mjini kupita Igundu mpaka Sangambia ambako itaunganisha na Mbarali kwa kipindi hiki imeharibika sana kutokana na changamoto za mvua. Je, ni Serikali itatenga fedha hili barabara hii ijengwe kwa kiwango cha changarawe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA ina bajeti ya bilioni 11 kwa ajili ya dharura na hivi sasa maombi tayari yamefanyika kwa ajili ya kuongeza bajeti hii kwenda bilioni 46 ili kuhakikisha wana fedha ya kutosha kuweza kutengeneza barabara hizi wakati wa dharura. Kwa sasa tutaangalia barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge kuona katika mwaka fedha unaoenda kuanza tarehe 1, Julai inapewa kipaumbele cha kutengenezwa.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 5

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Tuna ahadi ya Waziri wa TAMISEMI katika Wilaya ya Kibiti kutoa fedha kujenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kibiti Mjini kwenda kule kwenye Halmashauri yetu ya Kibiti.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha hizo kukamilisha ujenzi huo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri ya Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutakaa na wenzetu wa TARURA kuona ni namna gani wamejipanga katika kutekeleza ahadi ya hii ya Mheshimiwa Waziri ya kuweka barabara ya lami kutoka Kibiti Mjini mpaka ambapo wamejenga halmashauri yao. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mkato kati ya Wilaya za Mbarali na Chunya ili kupunguza gharama za usafiri na kukuza biashara?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ahadi ya Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu ni kuiunganisha Kata ya Nyahua na Makao Makuu ya Wilaya ya Sikonge na zilitengwa bilioni 1.86 mwaka juzi na mwaka jana, lakini haijatoka hata senti moja. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza hiyo ahadi kwa kutoa hizo fedha ambazo zilitengwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimeshawajibu Waheshimiwa Wabunge wengine hapa kwamba, kwa kuwa hii ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutakaa na wenzetu wa TARURA kuona ni namna gani wamejipanga katika utekelezaji wa ahadi hii.