Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa wa Hospitali Kongwe ya Magunga?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Spika, kimsingi hospitali yetu hii ni kongwe sana inawezekana ni kati ya hospitali kongwe zaidi Tanzania ambayo ilijengwa mwaka 1952.

Je, Serikali inatupa commitment gani kwamba tutapewa fedha hizi maana tumekuwa tukiahidiwa mara nyingi tunaletewa fedha za ukarabati na hatujawahi kupewa.

Je, Serikali ina tupa commitment gani kwamba fedha hizi zitakuja ili hospitali yetu hii ipate kukarabatiwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetoa majibu yangu ya msingi katika mwaka wa fedha 2023/2024 hospitali hii kongwe ya Mjini Korogwe ya Magunga imeshatengewa shilingi milioni 900 kwa ajili ya ukarabati.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa wa Hospitali Kongwe ya Magunga?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kijiji cha Idunda kata ya Kimara wamekarabati jengo lao wenyewe ili liwe zahanati na limekamilika.

Je, Waziri yuko tayari kuagiza Serikali kupeleka watumishi na vifaa tiba mara moja kwa sababu wanatembea zaidi ya kilometa 40 kupata huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwenye zahanati hii ya Idunda katika ajira hizi ambazo Serikali imetangaza za elimu na afya tutahakikisha kwamba zahanati hii inapata watumishi. Lakini vilevile kuhusu vifaa tiba naomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako hili kumuelekeza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo kuhakikisha anaanza kuweka fedha kwa ajili ya kununua vifaa tiba na sisi huku Wizarani tutaona ni lipi ambalo linaweza likafanyika ku-complement jitihada za Mkurugenzi wa Halmashauri.