Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuwa na Sera ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwenye Mikoa ya Kanda ya Kati?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msimu wa mwaka jana Mkoa wa Dodoma hatukupata mbegu za mtama mfupi lakini vile vile mbegu ya alizeti hatukupata na nataka kupata majibu ya Serikali. Serikali ina mkakati gani kwa msimu unaokuja ili kwanza tupate uhakika wa mbegu ambao tumekuwa hatupati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la jingine la pili ni kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba yapo mabwawa saba ambayo miongoni yatajengwa Dodoma. Je, mabwawa hayo ni yapi na yataanza kujengwa lini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza la kuhusu mbegu za alizeti na mtama mfupi nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika msimu ujao wa kilimo wakulima wa Mkoa wa Dodoma pia watanufaika na utoaji wa mbegu hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuhusu mabwawa. Katika jibu langu la msingi nimetamka mikoa mitatu kwa maana ya Tabora, Dodoma pamoja na Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabwawa ambayo tunayo mpaka yanaendelea hivi sasa ni mabwawa ya Msagali pale eneo la Mpwapwa, Bwawa la Membe ambalo litakuwa lina uwezo wa kuzalisha maji mita za ujazo milioni 12 lakini vile vile Lyamalwaga ambayo iko Nzega, vile vile Kongogo ambayo iko Bahi na mengine akiyataka kwa orodha nitamtajia yote katika Mkoa wa Dodoma, kwa sababu ya muda naomba niyataje haya machache. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuwa na Sera ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwenye Mikoa ya Kanda ya Kati?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza tija kwenye zao la korosho ambao kwa msimu uliopita imeuzwa kwa bei ya chini na ya kutupa na kuwaletea hasara wananchi wa Mtwara? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sera yetu ya Kilimo ya mwaka 2013 kipengele cha pili (2)(3) likiwa ni lengo la pili la malengo 10 ya sera ya kilimo imeeleza kuhusu tija katika mazao yote ya kilimo hapa nchini. Yako mambo lazima tuyafanye kama Serikali ili wakulima wetu waweze kulima kwa tija. Jambo la kwanza ni kuhakikisha tunapima afya ya udongo kutambua virutubisho ndani ya udongo ili tuwashauri vizuri wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili ni kuimarisha utafiti na cha tatu ni huduma za ugani na ugawaji wa pembejeo. Nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwenye korosho tunajua kuna changamoto nyingi na jana tulikuwa na kikao cha tathmini tumeyaona na tutayafanyia kazi ili wakulima wa korosho na wenyewe waweze kulima kwa tija tuweze kufikia malengo na matarajio ambayo tumejiwekea kama nchi.