Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara hiyo ndiyo inaelekea Makao Makuu ya Halmashauri. Kwa kujenga kilometa mbili kwa mwaka barabara ya kilometa 79; je, Serikali ina mkakati gani wa makusudi kabisa wa kuimaliza barabara hii kwa wakati kwa kuzingatia umuhimu wake? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Nataka Serikali inieleze kwa dhati ya moyo kabisa, inamaliza lini Barabara ya kutoka Mtwara Mjini kupita Tandahimba – Newala mpaka Masasi ile ya kilometa 210? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, Mtwara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii kweli ni ndefu na inaenda kwenye Makao Makuu ya Wilaya. Ndiyo maana tumeshaifanyia usanifu, lakini kadiri fedha inavyopatikana tumeona tuanze kuijenga wakati tunatafuta fedha ya kuijenga yote kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, dhamira ipo ndiyo maana tumeanza.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili, barabara ya kilometa 210 ya kutoka Mtwara – Mnivata – Newala hadi Masasi, Serikali imeshaanza kuijenga; kilometa 50 kutoka Mtwara hadi Mnivata, na sasa hivi tuko kwenye maandalizi ya kuanza kuijenga barabara yote kuanzia Mnivata hadi Masasi. Tumegawa lots mbili, kwa wahisani ya wenzetu wa African Development Bank ambao wanafadhili hiyo barabara, ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kujenga barabara ya Ramadhani – Iyai, Mkoani Njombe ambayo iko kwenye Ilani ya CCM kwa zaidi ya miaka 15?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii barabara ya Ramadhani
– Iyai tumeshaanza kuijenga kwa awamu. Mwaka huu nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeitengea pia fedha kwa ajili ya kuendelea kuijenga. Matazamio ya Serikali ni kuikamilisha barabara yote hii kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Kakonko – Kinonko – Guarama mpaka mpaka wa Muhange, ambayo ni barabara itakayounganisha Tanzania na Gitega, ambayo ni Makao Makuu mpya ya Burundi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zainab Katimba, Mbunge Viti Maalum, Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya kuanzia Kakonko hadi Muhange ni kweli inaunganisha Tanzania na Burundi na sasa hivi Makao Makuu yao yamesogea Gitega. Ilikuwa haijafanyiwa usanifu, lakini tutakamilisha usanifu ikiwa ni maandalizi kwa kuijenga barabara hii yote kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kibaoni – Majimoto – Inyonga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariki, Mbunge wa Viti Maalum, Katavi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilishatolewa ahadi na ipo kwenye Ilani. Naomba Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, tuone bajeti tutakayopitisha, naamini kuna mapendekezo ya kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami, kuunganisha Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Tabora, ahsante.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 5

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Karera – Munzeze – Janda hadi Buhigwe, kilometa 72 kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Karera – Muzenze hadi Buhigwe tayari ipo kwenye kukamilishwa kufanyiwa usanifu barabara yote ikiwa ni maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami. Tayari ipo kwenye usanifu na tupo kwenye hatua za mwisho, ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 6

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Lyazumbi inayounganisha Mkoa wa Rukwa na Katavi kupitia Mbuga ya Wanyama Katavi? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara hii ni barabara kuu, lakini kabla ya kuijenga hiyo barabara, ndiyo maana tumeamua kuijenga kwanza barabara ya Kizi – Kibaoni, Kibaoni kwenda Stalike. Kwa sababu hizo barabara zitakuwa zinakwenda parallel, baada ya kukamilisha, ndiyo sasa tutahamia pia kwenye hiyo barabara ambayo inapita katikati ya mbuga, ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 7

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya lami kutoka Airport kwenda Nyanguge yenye kilometa 47? Kwa sababu, upembuzi yakinifu umeshafanyika na barabara hii ni Bypass ya kupita Serengeti?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mwanza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni moja ya barabara ya Bypass katika Mkoa wa Mwanza, Airport – Igombe – Kayenze hadi Nyanguge. Namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, tuone bajeti hii tutakuwa tumepanga nini? Ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 8

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujua kwenye mwaka uliopita, katika bajeti Naibu Waziri, aliahidi kujenga barabara ya Bariri – Mgeta; je, sasa iko kwenye bajeti inayokuja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, barabara hii amekuwa anaifuatilia; na kwa kuwa bado hatujapitisha bajeti, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira tuone kama hii barabara tumeshaipangia bajeti. Mpango wa Serikali ni kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini barabara ya kilometa tano ya kutoka Kinyanambo C – Mapanda mpaka Kisusa, Jimbo la Mufindi Kaskazini, itajengwa? Kwa sababu hii barabara inafungua uchumi wa Mufindi Kaskazini.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge Viti Maalum, Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii aliyoitaja ni kweli inafungua uchumi, lakini ujenzi wake pia utategemea na upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kadiri fedha zitakavyokuwa zinapatikana, barabara hii itajengwa yote kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 10

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, barabara inayoanzia Wilaya ya Rorya inapita Susuni – Sirari – Mbogi – Nyansincha mpaka Nyanungu ni barabara ya kiusalama ambayo iko mpakani.

Nilitaka kujua barabara hii ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami ili kuweza kuimarisha usalama katika mpaka wa Tanzania na Kenya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri barabara hii kabla ya kuja Bungeni nimeipitia yote, na ikiwa ina mahitaji makubwa sana pia ya Mkoa wa Mara kwa maana ya usalama. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inaifanyia kazi kuhakikisha kwamba hii barabara inaimarishwa na kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.