Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Moja, barabara hii inaunganisha Mikoa Mitatu. Inaunganisha Mkoa wa Singida, Dodoma na Manyara. Naomba kujua ni kwa nini, barabara hii tusiipandishe hadhi iwe TANROADS ili iweze kuhudumiwa kwa urahisi zaidi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Naibu Waziri Jimbo Lake na Jimbo langu linaunganishwa na barabara chafu kweli kweli, kati ya Seya na Zajiro kwake. Nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha barabara hiyo inatengenezwa? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu kupandisha hadhi barabara hii ambayo inaunganisha Mikoa Mitatu ya Singida Dodoma na Manyara, utaratibu upo wa kisheria kwa maana lazima vikao vianze katika ngazi ya Wilaya, vikitoka kwenye Wilaya viende kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa na baada ya kutoka Bodi ya Barabara ya Mkoa viende RCC na ndipo hadhi ya barabara hii iweze kupandishwa.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili. Nikiri ni kweli barabara hii inayounganisha kati ya Jimbo la Mheshimiwa Monni na Jimbo langu mimi la Chamwino na tayari maelekezo yalikuwa yameshakwenda kwa Mameneja wote wa TARURA wa Mikoa, kuhakikisha kwamba wanatenga fedha ya kuhakikisha vipande vya barabara hii vinaanza kutengenezwa. Katika mwaka huu wa fedha tuliouombea wa 2023/2024 barabara hii vilevile imo katika barabara zilizoombewa fedha. Naomba kuwasilisha.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kukarabati barabara ya kuanzia Bwakila Chini mpaka Bwakila Juu katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini ili iweze kupitika bila ya matatizo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Dkt. Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha kadri ya upatikanaji wa fedha kwenye bajeti kwa ajili ya ukarabati wa barabara. Ninaomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro na Meneja wa TARURA Wilaya ya Morogoro Vijijini kuhakikisha kwamba wanaenda kuiangalia hii barabara na kuona kama imetengewa fedha kwenye bajeti hii ambayo tumetoka kuiombea na Bunge lako Tukufu imepitisha ili kama ilitengewa fedha basi ukarabati wake uanze mara moja.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Kutokana na mvua zinazoendelea barabara ya kutoka Kitoho kwenda Mwatasi inayounganisha na Masisiwe kwa sasa imepata madhara makubwa na haipitiki.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha za dharura ili barabara hii iweze kupitika vizuri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyamoga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natoa tena maelekezo tena hapa kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI kwa Meneja wa TARURA Mkoa wa Iringa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilolo kuweza kwenda kuifanyia tathmini barabara hii ya Mwatasi - Kilolo na kuona maeneo ambayo yameathirika sana ili waweze kuyafanyia kazi kwa haraka.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuweza kuniona. Barabara ya kutoka Matundasi kuelekea Itumbi imeharibika sana baada ya mvua hizi ambazo zinazoendelea kunyesha.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha ili barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha changarawe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka, Mbunge wa Chunya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Matundasi mpaka Itumbi ni kweli ipo chini ukilinganisha na usawa wa barabara yenyewe na ardhi ya pembezoni, tayari katika mwaka huu wa fedha wa 2023/2024 barabara hii imeombewa fedha na ukarabati wake utaanza ili kuweza kuinyanyua.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 5

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri ni lini Serikali itaanza kujenga kwa lami barabara ya Tabora Mambari ili kuunganisha Tabora Magharibi na Mashariki?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Almas Maige kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara hii unategemeana na upatikanaji wa fedha na tutaangalia katika bajeti hii ambayo imepitishwa ambapo ninyi Bunge hili Tukufu limeiidhinishia TARURA matumizi uya fedha ya zaidi ya Bilioni 830, kwa ajili ya kuweza kukarabati barabara mbalimbali nchini mwetu kwenye Majimbo yetu ikiwemo Jimbo la Mheshimiwa Almas Maige, kwa hiyo tutaliangalia na kuweza kulifanyia kazi.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Makamu wa Rais alivyokuwa Shinyanga aliahidi barabara ya kutoka Ndala kwenda Mwawaza ambako kuna Hospitali ya Rufaa, ingetengenezwa kwa kiwango cha lami.

Ningependa kujua ni lini itaanza kutengezenzwa kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge barabara hii ni ahadi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vilevile inaunganisha huduma muhimu kwenye jamii kama vile Hospitali hii ambayo iko hapo, hivyo basi Serikali itaipa kipaumbele na kutekeleza utekelezaji wa barabara hii kama ilivyokuwa maelekezo ya Makamu wa Rais lakini vilevile ni uhitaji mkubwa wa wananchi wa Shinyanga.